Umoja wa mataifa waidhinisha kupeleka askari zaidi Juba

un1
Kikosi kipya cha wanajeshi kutoka Afrika kitaweza kukabiliana na wale wanaowatishia raia
un2
Maelfu ya raia walilazimika kutafuta hifadhi katika ofisi za Umoja wa Mataifa wakati wa mapigano ya mwezi Julai
CHANZO BBC
………………………………………………………………………………………
Baraza la usalama la Umoja wa Mataifa limesema linajiandaa kuiwekea Sudan kusini vikwazo vya silaha , ikiwa itajaribu kuzuia kupelekwa kwa wanajeshi wa ziada wa kulinda amani nchini humo.
Hata hivyo Bw Kiir amesema hataruhusu Umoja wa Mataifa kuchukua udhibiti wa nchi yake na hatashirikiana tena na umoja huo. Kikosi hiki cha Umoja kitakachoundwa na askari wa Afrika kitakuwa na majukumu makubwa zaidi ya askari zaidi ya 12,000 wa Umoja wa Mataifa ambao wako tayari katika taifa hilo.
Mapigano baina ya vikosi hasimu ya mwezi Julai yaliwauwa mamia ya watu na wengine maelfu kadhaa kuyakimbia makwao.
Vikosi vya Umoja wa Mataifa vinakabiliwa na kazi ngumu ya kuwalinda raia ambapo zaidi ya watu 35,000 walikimbilia kwenye makao makuu yake mjini Juba.
Tofauti na kikosi cha kulinda amani kilichopo nchini humo kikosi cha Afrika kitakachokua chini ya Umoja wa Mataifa kitaweza kukabiliana na wale watakaowatishia raia
Hata hivyo haijawa wazi ikiwa kikosi hich
ilichopo nchini humo, kikosi cha Afrika kitakachokua chini ya Umoja wa Mataifa kitaweza kukabiliana na wale watakaowatishia raia
Hata hivyo haijawa wazi ikiwa kikosi hicho kitaweza kufanya kazi bila ushirikiano na Sudan kusini.
Zaidi ya raia 100,000 wa Sudan kusini kwa sasa wamekimbilia katika nchi jirani kufuatia mapigano ya hivi karibuni, linasema shirika la la wakimbizi la Umoja wa Mataifa.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni