Viongozi wa UVCCM  mkoa wa Arusha wakiwa wanatembelea shule ya Sekondari ya NaNja ilioungua na moto July 2 mwaka huu 
 mwenyekiti wa
 UVCCM mkoa wa Arusha Sabaya Lengai wa pili kushoto akiwa anaangalia bweni la shule ya Nanja lililoungua na moto

 Mwenyekiti  wa UVCCM Arusha akiwa na 
wanafunzi wa shule ya Sekondari ya Nanja ilioungua na moto hivi karibuni
 wakati alipoenda kutembelea shule hiyo na kutoa mifuko 100 ya  simenti 
kwa ajili ya ujenzi wa bweni la shule hiyo lililoungua na moto
Na Mahmoud Ahmad,Arusha 
Umoja
 wa vijana Wa chama cha mapinduzi Mkoa wa Arusha wamehaidi mifuko 100 ya
 simenti kwa ajili ya ujenzi wa  shule ya sekondari Nanja iliopo 
wilayani Monduli  mkoani Arusha iliyounguliwa bweni  na moto mapema july
 2 mwaka huu
Akiongea
 na wanafunzi wa shule hiyo mwenyekiti wa UVCCM mkoa wa Arusha Sabaya 
Lengai alisema kuwa wao kama vijana wa ccm mkoani hapa wameguswa sana na
 tukio hilo ndio maana wakaamua kujikusanya na kwenda kutembelea shule 
hiyo pamoja na kuwapa mifuko 100 ya simenti kwa ajili ya ujenzi wa bweni
 ambalo limeungua.
Alisema
 kuwa wao kama vijana wanamoyo na wananguvu hivyo wako tayari kuwasaidia
 wadogo zao ambao wapo mashuleni na ndio maana wameamua kutoa mifuko 
hiyo.
"unajua
 atuna ela nyingi lakini tumeamua kuwapa msaada hawa wadogo zetu ili 
wasome  kwa raha na wasiwe na mawazo kabisa kuhusia na tatizolililo 
wakuta na ndio maana wameamua kuwapa msaada huo"alisema Sabaya 
Alisema
 kuwa mchawi hatoki mbali ivyo ni wajibu wa kila mwanafunzi kufanya 
uchunguzi na iwapo ata jua nani alisababisha bweni hilo likaungua watoe 
taarifa katika ngazi usika.
Aliwatoa
 hofu wanafunzi hao kwa kuwasihi wasiwe na wasiwasi wa kuishi shuleni 
hapo kwani serekali ya chama cha mapinduzi chini ya Rais wake John 
Magufuli ipo makini katika swala zima la ulinzi na imeimarisha ulinzi 
shuleni hapo hivyo wasome wakiwa na amani kabisa wakijua kuwa kunawatu 
wanawalainda.
Kwa
 upande wake katibu wa UVCCM wilaya ya Arusha Ezekiel Molel aliwasihi 
wanafunzi hao kuzingatia masomo kwani amna urithi wowote wanaoweza 
kupewa na walimu wao zaidi ya elimu
Aliongeza
 kuha haya yanayotokea ni matatizo ya kawaida ivyo wasiyaweke akilini 
bali waangalie swala la kusoma na fate sana elimu maana bila elimu amna 
kitu chochote ambacho wanawezakukipata katika miaka hii .
"serekali
 ya sasa hivi aina mambo ya kona kona hivyo wadogo zangu naomba niwasihi
 msome sana mzingatie elimu maana bila elimu hamna kitu chochote 
kinachoweza kufanyika kwanielimu ni kila kitu kwa kipindi hata 
mnavyotuona sisi hapa sisi wenyewe  tumesoma na tunakazi na ndio maana 
leo hii tumeweza kuja kuwapa pole na kuchangia hiyo mifuko 100 tungekuwa
 atuna elimu hata kuja hapa au kufanya hizi kazi tusingeweza "alisema 
Molell
Aliwaambia
 kuwa ata vitabu vya dini vimeaandika waishikilie sana elimu na 
wasiiacha iende zake hivyo ni wajibu wao kuweka akili zao katika swala 
zima la elimu na sio kungine ,aliongeza kuwa sasa ivi kuna gonjwa hatari
 la ukimwi hivyo ni wajibu wao wanafunzi ambao ni taifa la kesho 
kuhakikisha wanaepuka vishawishi mbalimbali ambavyo vinaweza jitokeza







Hakuna maoni:
Chapisha Maoni