MBUNGE WA ARUSHA MJINI MBARONI KWA UCHOCHEZI

Image result for mbunge arusha mjini picha 

Na Mahmoud Ahmad Arusha
JESHI la polisi mkoa wa Arusha linamshikilia mbunge wa jimbo la Arusha Mjini  Godbless Lema (CHADEMA) kwa tuhuma za kutoa na  kusambaza maneno ya uchochezi katika mitamndao mbalimbali ya kijamii.
 
Akithibitisha kukamatwa kwa mbunge  Lema mbele ya vyombo vya habari kamanda wa polisi mkoa wa Arusha Charles Mkumbo alisema Lema alikamatwa jana majira ya saa 12;00 asubuhi nyumbani kwake Njiro akiwa amelala.
Alisema baadhi ya menono hayo ni “Kama mauti imepoteza utukufu wake hakuna statement ya kurudisha nyumba Arusha kuandamana”
 
Kwa mujibu wa kamanda maneno hayo aliyotoa Lema ni ya uchochezi na kuvuruga amani ya nchi na ndiyo maana wanamshikilia kwa ajili ya mahojiano juu ya kaluli zake hizo
.
Alisema watanzania wanatambua umuhimu wa amani na hakuna mtu aliyejuu ya sheria hivyo ni vyema tukaheshimu amani na utulivu tulionao.
Aidha alisema utii wa sheria bila shurti ni vyema ukazingatiwa ili kuepuka machafuko ambayo yanaweza kutokea kutokana na maneno hayo ya uchochezi.
Hata hivyo polisi baada ya kumkamata  wameifanyia upekuzi nyumba yake ili kubaini iwapo kuna vitu vyenye kuashiria uchochezi zikiwemo fulana ama bendera zenye maandishi ya  Ukuta.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni