KISHINDO CHA UZINDUZI WA MSIMU WA TIGOFIESTA 2016 CHAZIZIMA JIJINI MWANZA USIKU WA JANA

 
Mkali wa singeli ManFongo na Shilole wakilivamia jukwaa la Tigo Fiesta 2016 katika tamasha hilo kubwa liliofanyika usiku wa jana jijini Mwanza na kukutanisha wasanii nguli katika muziki wa kizazi kipya na Msanii wa kimataifa toka Nijeria Wizkid . 
Umati wa wakazi wa Jiji la Mwanza wakitoa shangwe wakati burudani mbalimbali zikiendelea katika Tamasha la Tigo Fiesta 2016 viwanja vya CCM Kirumba hapo usiku wa jana. 
Alikiba alikuwa kivutio kwa mashabiki wengi mara baada ya kufanya suprize na kutoa burudani ya kukata na shoka huku mashabiki zake wakifuatisha nyimbo zake moja baada ya nyingine katika Tamasha la Tigo Fiesta 2016 katika viwanja vya Kirumba Jijini Mwanza.  
Benpol akilishambulia jukwaa la Tigo Fiesta 2016 lilifnayika jana katika viwanja vya CCM kirumba Jijini Mwanza.  
Msanii wa kizazi kipya Dayna Nyange akitumbuiza umati uliohudhuria Tamasha la Tigo Fiesta 2016 jijini Mwanza hapo usiku wa jana.
 
Mkali wa Singeli anayetamba na nyimbo yake “HAINAGA USHEMEJi” akitumbuiza jukwaa la Tigo Fiesta 2016 Jijini Mwanza. 
Aika na Nahreel (Navykenzo ) nao walifanikiwa kuteka jukwaa la Tigo Fiesta 2016 Jijini Mwanza  
Wasanii toka kikundi cha TipTop connections Tundaman na Madee Ali wakitumbuiza mashabiki katika jukwaa la Tigo Fiesta 2016 katika viwanja vya CCM kirumba hapo usiku wa jana .  
Weusi wakilishambulia vilivyo jukwaaa la Tigo Fiesta 2016 Jijini Mwanza hapo usiku wa jana  
Msanii wa kimataifa toka Nigeria Ayodeji Balogun(Wizkid) akitumbuiza katika tamasha la Tigo Fiesta 2016 liliofanyika hapo jana Jijini Mwanza katika viwanja vya CCM Kirumba  
Baadhi ya waandishi wa Habari wakichukua matukio katika tamasha la Tigo Fiesta 2016 wakazi msanii wa kimataifa toka Naijeria Wizkid akitumbuiza katika viwanja vya CCM kirumba usiku wa jana .  
Baadhi ya wakazi wa jiji la Mwanza wakishangilia wakati burudani mbalimbali zikitolewa na wasanii waliotikisa jukwaaa la Tigo Fiesta 2016 hapo usiku wa jana katika viwanja vya CCM Kirumba Jijini Mwanza

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni