SAED Kubenea Mbunge wa Jimbo la Ubungo jana alijisalimisha Kituo Kikuu 
cha Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam na kuhojiwa kabla ya kupewa 
dhamana kufuatia tuhuma za kuandika makala inayodaiwa kuwa ya uchochezi 
kuhusu hali ya kisiasa Zanzibar.
Kubenea ambaye anadaiwa kufanya uchochezi kwa kuandika makala katika 
gazeti la MwanaHALISI toleo la 349 la Julai 25-31 yenye kichwa cha 
habari, ‘Yuko wapi atakayeiokoa Zanzibar?’
Kubenea alifika katika kituo hicho cha Polisi jana  saa saba na robo 
mchana (13:15) akiwa na Tundu Lissu Mwanasheria Mkuu wa Chama cha 
Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) pamoja na Frederick Kihwelu wakili 
mwandamizi wa Chama hicho.
Baaada ya kuhojiwa kwa zaidi ya masaa mawili, saa tisa na robo alasiri 
(15:45) alitoka na kuondoka huku wandishi wa habari wakishindwa 
kuzungumza naye baada Jeshi la Polisi kuwazuia waandishi wa habari 
kuingia katika eneo la kituo hicho.
Akizungumza kwa njia ya simu, Lissu ambaye ndiye mwanasheria wa Kubenea 
katika sakata hilo alisema kuwa, Kubenea amehojiwa kwa madai ya 
uchochezi lakini alichokiandika ni hali halisi ya Zanzibar hususani 
visiwa vya Pemba.
“Kubenea amechiwa kwa dhamana na ameamriwa kurudi tena kituoni hapo tarehe 18 Agosti, mwaka huu,” alisema Lissu.
Katika makala yake inayodaiwa kuwa ni ya kichochezi iliyokuwa na kichwa 
cha habari, “Yuko wapi atakayeiokoa Zanzibar?” Kubenea alielezea jinsi 
Jeshi Polisi Visiwani Pemba wavyonadaiwa kuwabambikia kesi wananchi, 
kuwapiga na kuwatesa kwa madai kuwa wananchi hao wanaipinga serikali.
Kubenea aliandika Makala hiyo baada ya kusafiri kutoka Dar es Salaam 
Mpaka Zanzibar kufuatilia kile alichokitaja kama mateso, unyanyasaji na 
ukiukwaji wa haki za binadamu dhidi ya wananchi wasio na hatia visiwani 
humo.
Miongoni mwa vijana na wahanga wa kubambikiwa kesi, kupigwa na kuteswa 
visiwani Pemba waliotajwa na Kubenea katika makala yake ni ni Hijja 
Hassani aliyetangazwa kuwa ni Mwakilishi wa Jimbo la Kiwani kabla ya 
Jecha Salim Jecha Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) kufuta 
uchaguzi.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni