Nyota wa Mpira wa Pete wa Tanzania
 Mwanaidi Hassan (GS) akiwa katika hekaheka za kuisaidia Timu yake 
kupata Ushindi katika mashindano ya Majeshi kwa Nchi za Afrika Mashariki
 inayoendelea katika Uwanja wa Amahoro Kigali ambapo katika Mchezo huo 
Tanzania iliifunga Rwanda 56-13(Picha na Dora Mushi) .
Nyota Chipukizi wa  Mpira wa Pete 
wa Tanzania Nasra Suleiman ( Mwenye  Mpira)akiwa katika hekaheka za 
kuisaidia Timu yake kupata Ushindi katika mashindano ya Majeshi kwa Nchi
 za Afrika Mashariki ambapo katika Mchezo huo  uliofanyika katika Uwanja
 wa Amahoro Tanzania iliifunga Rwanda 56-13(Picha na Dora Mushi) .
Kocha wa Timu ya Tanzania kwa 
Mpira wa Pete Argentina Daudi akitoa maelekezo kwa Wachezaji wake katika
 muda wa mapunziko katika mchezo baina yao na Rwanda  uliofanyika katika
 Uwanja wa Amahoro Kigali  ambapo Tanzania iliifunga Rwanda 56-13(Picha 
na Dora Mushi) .
Mlinzi wa Timu ya Mpira wa Pete wa
 Tanzania Joyce Kaira (GK) akiwa katika hekaheka za kuzuia Wachezaji wa 
Rwanda  Timu yake kupata Ushindi katika mashindano ya Majeshi kwa Nchi 
za Afrika Mashariki ambapo katika Mchezo huo uliofanyika katika uwanja 
wa Amahoro  Tanzania iliifunga Rwanda 56-13(Picha na Dora Mushi) .
Mchezaji wa Mpira wa Pete wa 
Tanzania Nasra Suleiman ( GA)akiwa katika harakati za kuifunia Timu yake
 katika mashindano ya Majeshi kwa Nchi za Afrika Mashariki katika Uwanja
 wa Amahoro Kigali  ambapo katika Mchezo huo Tanzania iliifunga Rwanda 
56-13(Picha na Dora Mushi) .
Mchezaji wa Mpira wa Pete wa 
Tanzania Nasra Suleiman ( GA)akiwa katika hekaheka za kuisaidia Timu 
yake kupata Ushindi katika mashindano ya Majeshi kwa Nchi za Afrika 
Mashariki yanayoendelea katika uwanja wa Amahoro Kigali Rwanda ambapo 
katika Mchezo huo Tanzania iliifunga Rwanda 56-13(Picha na Dora Mushi) .
Kikosi cha Mpira wa Miguu cha 
jeshi la Wananchi wa Tanzania wakiwa katika picha ya pamoja Muda mfupi 
kabla ya Kuanza kwa mchezo wao dhidi ya Kenya uliofanyika katika Uwanja 
wa  Nyamirambo Rwanda ambapo Tanzania iliibuka na Ushindi wa Bao 2-1.
……………………………………………………………………………………
Na Selemani Semunyu JWTZ
Timu ya Mpira wa Pete ya Jeshi 
la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania imedhihirisha Ubabe wake katika mchezo
 huo baada ya kuifunga Timu ya Jeshi la Rwanda RDF kwa Magoli 56-13 
kiwango ambacho hakijawahi kufikiwa na Timu zote tangu kuanza Mashindano
 hayo.
Tangu Mwanzo wa Mchezo huo 
uliofanyika katika Uwanja wa Amahoro Rwanda walionekana kuzidiwa na 
kiwango kilichoonyeshwa na Tanzania kupitia Nyota wake Mwanaidi Hassan 
aliyefunga 37 na Nasra Suleiman aliyefunga 19 waliokuwa mwiba kwa Timu 
ya Rwanda kutokana na kupachika magoli kila wapatapo mpira.
Tanzania iliweza kumiliki 
vipindi vyote vine vya mchezo huku Rwanda wakionekana kutoelewana 
kutokana na idadi ya magoli waliokuwa wakifungwa tangu Robo ya Kwanza 
mbayo ilimalizika kwa Tanzania kuongoza kwa 13-2 huku Robo ya pili 32-6 
na Robo ya tatu 42-10.
Kwa upande wake Mchezaji Nasra 
Suleiman alisema mbali na kupata ushindi huo lakini hawatobweteka kwani 
wanawasubiri Kenya ili kutangaza Ubingwa kwa kushinda Michezo yote.
Kwa upande mwingine Tim u ya 
Mpira wa Miguu ya Tanzania wameinyamazisha Timu ya Jeshi ya Kenya baada 
ya kuwafunga mabao 2-1 katika mchezo uliofanyika katika Uwanja wa Kigali
 Nyamirambo.
Katika Mchezo huo Kenya Ndio 
walianza kupata bao  Muda mchache kabla kwenda mapumziko katika Dakika 
ya 42 kupitia kwa mchezaji wake  Private Peter Onyango  kabla ya Dakika 
tatu Baadae Private Prosper  Mkwama kusawazisha bao na kwenda mapumziko 
wakiwa Sare.;
Kipindi cha Pili kilianza huku 
Timu zote zikifanya mabadiliko na kosa kosa ya magoli kwa Nyakati 
tofauti lakini Mnamo dakika ya 77 Private Abdulrahman Musa akaiandikia 
Tanzania bao la Pili na la ushindi.
Kufuiatia matokeo hayo sasa 
Tanzania wamebakiza Mchezo mmoja na Rwanda utakaopigwa siku ya ufungaji 
 Agosti 17 katika Uwanja wa Amahoro huku Timu ya mpira wa Pete 
wanatarajia kukutana na Kenya Agosti 14
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni