STARTIMES YAANDAA SHINDANO LA KUKUZA VIPAJI VYA SAUTI DAR,ARUSHA NA ZANZIBAR KESHO

 Picha ikionyesha Tangazo la shindano la kukuza vipaji vya sauti lililoandaliwa na serikali na kampuni ya ving'amuzi ya Startimes ambapo shindano hilo linatarajiwa kufanyika kesho kwenye ukumbi wa Triple A  kwa mkoani Arusha.
  Meneja wa Kampuni ya Startimes Tawi la Arusha pichani akizungumza na wanahabari kutoka vyombo mbalimbali ofisini kwake ambapo alizungumzia kampuni hiyo kwa kushirikiana na serikali wameandaa shindano la kukuza vipaji vya sauti hapa nchini shindano litakalofanyika katika mikoa Mitatu ya Arusha,Dar es Salaam na Zanzibar.
PICHA JUU NA CHINI  WAANDHISHI WA HABARI WAKIWA KAZINI KUAPATA MATUKIO MBALI MBALI KWENYE OFISI ZA STARTIMES JIJINI ARUSHA LEO .

 Pichani ni viongozi wa kampuni ya Startimes tawi la Arusha wakionyesha baadhi ya zawadi ambazo washiriki na washindi watajinyakulia hiyo kesho kwenye ukumbi wa Triple A jijini Arusha.

 Tv inayoonekana kwenye picha ni zawadi itakayonyakuliwa na washindi wa shindano hilo kesho katika mikoa mitatu ya Dar es salaam,Arusha na Zanzibar.

Picha ikionyesha Tangazo la shindano la kukuza vipaji vya sauti lililoandaliwa na serikali na kampuni ya ving'amuzi ya Startimes ambapo shindano hilo linatarajiwa kufanyika kesho kwenye ukumbi wa Triple A  kwa mkoani Arusha

Na Mahmoud Ahmad Arusha
StarTimes wameanda mashindano ya kusaka vipaji vya sauti kwa watanzania ambapo shindano hilo linaanza leo hapa jijini Arusha,Dar es Salaam na Zanzibar ambapo washindi watano kutoka kila mkoa wataungana  jijini Dar es salaam.
Akizungumza na wanahabari mbali mbali meneja masoko wa kampuni hiyo Ally ngozi alisema kuwa shindano hilo limeandaliwa na kampuni yao madhumuni yakiwa ni kukuza vipaji na kuwapatia ajira washindi.
Ngozi alisema kuwa kampuni hiyo kwa kushirikiana na serikali wameleta shindano hilo la sauti lengo likiwa ni kupunguza tatizo la ajira na kuibua vipaji ambapo mbali na ajira wahindi watajinyakulia Tv,Kingamuzi na simu za mkononi.
Alisema kuwa washiriki wa shindano hilo ni watanzania wote bila kujali umri wa jinsia ambapo kwa Arusha fomu zitatolewa kesho kwenye ukumbi wa Triple A uliopo sakina ambapo pia shindano litafanyikia hap siku hiyo
Aidha alisema kuwa washindi watano watakao patikana watakuwa wamejizolea ajira ya kufanyakazi katika kampuni hiyo.
“Nawasihi wakazi wa jiji la Arusha,Dar es salaam na Zanzibar kuachangamkia fursa hiyo ya kuwa mmoja wa washindi wa shindano letu la kukuza vipaji vya sauti” alisema Ally


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni