Na
 Augustus Fungo, Balozi wa Usalama Barabarani
HIVI karibuni imejitokeza njia mpya ya kusaidia kupambana na wimbi la 
ajali za barabarani, ambapo pamoja na faini kwa madereva wanaokiuka 
sheria za barabarani wamekuwa wakipigwa picha na baadaye picha hizo 
kuwekwa kwenye mitandao ya kijamii au magazetini na hata wakati mwingine
 kwenye televisheni. Mathalani katika mtandao wa facebook kundi la 
Mabalozi wa Usalama Barabarani maarufu kama, RSA wakishirikiana na Jeshi
 la Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani hutumia mbinu hii kuwapiga 
picha wakiukaji wa sheria za barabarani kisha kuzituma katika Kituo cha 
Mawasiliano cha Usalama Barabarani (Traffic Control Center, TCC).
 Kituo
 hiki huwatumia picha hizi ambazo pia ni ushahidi askari waliopo katika 
vituo mbalimbali barabarani, ili kuwezesha watuhumiwa kukamatwa na 
magari husika. Baada ya kukamatwa magari husika askari humwandikia faini
 mkosaji, kumpiga picha na kuituma kwenye kituo cha mawasiliano ya 
polisi (TCC) ambacho na chenyewe hutoa mrejesho kwa watoa taarifa.
 Picha
 hizo hatimaye kuwekwa kwenye mtadao wa facebook, hutumika kuandaa 
vipindi vya televisheni vya kuelimisha jamii mfano, ni kipindi cha ‘Aibu
 yako' kinachorushwa na televisheni ya ITV na pia picha hizo huhifadhiwa
 na kikosi cha usalama barabarani kwa ajili ya kumbukumbu na rejea iwapo
 dereva husika atarudia kosa hilo.
Njia hii mpya ambayo inaitwa kutaja na kuaibisha, ama kwa kiingereza 
“Naming and Shaming” ni maarufu sana inayotumika si tu na nchi nyingi za
 Ulaya bali pia na mashirika ya haki za binadamu kama 'Human Rights 
Watch', hutumia kuyaaibisha mataifa yaliyokubuhu kwa ukiukaji wa haki za
 binadamu. 
Saudi Arabia kupitia sheria yake ya makosa ya mtandao (Anti-cyber-crime 
law (Royal Decree No. M/17 dated 8 Rabi1 1428) imepitisha mbinu hii kama
 mojawapo ya adhabu. Mbinu kama hii hutumika pia katika nchi nyingi za 
Ulaya kuwaaibisha watu au makampuni yanayokwepa kodi. Moja ya makampuni 
yaliyowahi kuathirika na kadhia hii ni kampuni ya Kahawa ya Starbuck. 
Januari 15, 2015, serikali ya Uingereza iliwataja na kuwadhalilisha 
waajiri 37 wa Uingereza walioshindwa kulipa kima cha chini kwa 
wafanyakazi wao. 
Hata hivyo, mwandishi James Meernick(2012), anaitaja njia hii kama 
chaguo kuu la mashirika mengi ya kimataifa katika kuhakikisha haki za 
binadamu zinazingatiwa.
Njia hii hutumika ikiaminika kwamba kumuweka mtu au taasisi hadharani 
ili aweze kujiona mwenyewe, aonwe na familia yake, marafiki zake, na 
hata waajiri wakati akitenda kosa inasaidia kumfanya mtu ajitafakari na 
kutorudia kosa au pia kuwafanya wanaomzunguka kumpa shinikizo la kufuata
 sheria au kuheshimu haki za wengine. 
 Baadhi ya magari yanayopigwa picha njiani na raia wema na mabalozi wa 
usalama barabarani yakifanya makosa na picha zao kutumwa kituo cha 
mawasiliano cha kikosi cha usalama barabarani
Pamoja
 na hayo baadhi ya wadau nchini wameipokea mbinu hii kwa hisia tofauti. 
Wengine wamedai kwamba ni kinyume cha sheria japokuwa hawajaweka kutaja 
ni sheria gani hasa inayokiukwa kwa kufanya hivyo; wengine wamedai ni 
kuingilia usiri(privacy) ya mtu bila kusema ni kwa vipi siri ya mtu 
inaingiliwa pale anapotenda kosa. Pia wameshindwa kuushawishi umma 
kuelewa je, mtu anapokuwa mathalani anatanua barabarani (matumizi mabaya
 ya barabara), au analipita gari pasiporuhusiwa au anakimbia kwa zaidi 
ya mwendo kasi wa 80 (speed) kinyume na sheria akakamatwa akapigwa picha
 ni kwa jinsi gani anadhalilishwa zaidi ya kuaibishwa? 
Maana wakati anapigwa hiyo picha kwanza anakuwa ameshakubali kosa; pili,
 anakuwa hajavuliwa nguo wala kurushwa kichurachura, kupigwa au kufungwa
 pingu. Isitoshe wapinzani wa mbinu hii wameshindwa kuwashawishi 
Watanzania kuelewa iwapo kumpiga picha mkosaji barabarani ni kosa, 
inakuwaje au ni mara ngapi watuhumiwa wamekuwa wakipigwa picha 
wanapofikishwa mahakamani? 
Je, ni mara ngapi kumekuwa na matukio mfano ya ujambazi na watuhumiwa wa
 ujambazi katika eneo la tukio au walipokamatwa vyombo vya habari 
vimekuwa vikiwapiga picha. Je, huku si kuvunja sheria? Itakumbukwa Kituo
 cha Luninga cha ITV na vingine nchini vimewahi kurusha kipindi maalumu 
kinachoonesha askari wanaodaiwa wanapokea rushwa, mbona hili 
halikusemewa? Ni mara ngapi polisi wamekuwa wakitoa picha wa watu 
wanaotafutwa kwa uhalifu (wanted), ni mara ngapi waajiri wamekuwa 
wakitoa picha za wafanyakazi wao waliofukuzwa kazi kwa makosa ya 
kutokuwa waaminifu? Iweje leo picha za wakosaji wa barabarani tu 
tutolewa ionekane wanadhalilishwa?
Wapo watu wametoa hoja kuwa dereva mkosaji ana maisha yake mengine eti 
yanaathirika kutokana na kupigwa picha. Kimsingi hoja hii haina mashiko 
kwakuwa lengo la mbinu ya kutaja na kuaibisha ni kumfanya muhusika aone 
aibu kwa upuuzi alioufanya na kuweza kujirekebisha. Dereva anayejua kuwa
 hiyo inaweza kumuharibia hadhi yake huko baadae atakuwa makini zaidi 
kutokiuka sheria za barabarani au kuchezea maisha ya watanzania wasio na
 hakia. 
 Picha kama hii inaweza kutumwa katika kituo cha cha taarifa cha kikosi cha usalama barabarani kwa hatua zaidi
 Baadhi ya Mabalozi wa Usalama Barabarani maarufu kama, RSA
Gari
 za serikali, mashirika ya umma, miradi, na zinginezo haziko juu ya 
sheria. Bila kujali operesheni wanayofanya au lengo la safari yao 
hawapaswi kuvunja sheria, na endapo watakuwa wamevunja sheria kwa sababu
 ya kwenda kuhudhuria dharula husika, askari aliyesimamisha hilo gari 
akiridhika na sababu hiyo hata toza faini wala kupiga picha, kwa hiyo 
hakuna kitakachoathirika. Na endapo kuna hofu ya matumizi mabaya ya hizo
 picha, atakaye wajibika ni huyo anayetumia vibaya picha hiyo ili mradi 
tu picha halisi (original) ya tukio zima ipo na ndiyo itakayotumika kama
 ushahidi dhidi ya mtu aliyeitumia picha vinginevyo.
Ni ushauri wetu kuwa askari waendelee na mbinu hii ili wavunja sheria 
waaibike na kuweza kujirekebisha. Haiwezekani dereva amesomea 
amejaribiwa na kupewa leseni, anajua amebeba abiria kwenye gari lake 
halafu aendeshe kwa mwendo hatarishi, ayapite magari mengine kana kwamba
 amebeba viazi, au abiria ni mateka wake. 
Faini peke yake hazi saidii. Binafsi ningependa hata siku moja mahakama 
imhukumu mkosaji kufagia barabara za Kariakoo kwa wiki zima badala ya 
kumpeleka jela hii ingesaidia zaidi kurekebisha watu. Kimsingi ipo haja 
kama taifa tuwe na adhabu mbadala. Na kwa kuwa hakuna sheria inayovunjwa
 kwa mtu kupigwa picha wakati akitenda kosa na kuwekwa hadharani, mbinu 
hii bado itaendelea kuwa sahihi ili wahusika waache kutenda makosa 
ambayo yanagharimu si tu maisha ya watanzania bali pamoja na uchumi wa 
nchi. Naimani Jeshi la Polisi ni Jeshi lenye ueledi na wataalamu 
mbalimbali hivyo litaendelea kubuni mbinu mbalimbali za kurekebisha 
tabia na kutekeleza sheria. Hii ndio imani yangu kwa taasisi hii muhimu 
nchini Tanzania, wananchi tushirikiane nao.
Usalama Barabarani ni Jukumu Letu sote.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni