Mkuu
 wa Kambi ya Wakimbizi Nyarugusu iliyopo wilayani Kasulu, mkoani Kigoma,
 Sospeter Christopher Boyo (aliyesimama mwenye shati la kitenge) akisoma
 taarifa fupi ya Kambi ya Nyarugusu kwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya 
Nchi, Mh. Mathias Chikawe (aliyeketi mwenye suti ya kijivu) 
aliyeambatana na Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na 
Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro 
Rodriguez mara baada ya kuwasili kwenye kambi hiyo kujionea hali halisi 
ya mazingira na changamoto zinazowakabili Waomba hifadhi wa Burundi na 
Kongo. (Picha zote na Zainul Mzige wa modewjiblog)
Na Modewjiblog team, Kigoma
WAKATI
 dunia kupitia Mashirika ya Umoja wa Mataifa yanahangika kutanzua 
changamoto za wakimbizi Nyarugusu, mkoani Kigoma imeelezwa kuwa idadi 
kubwa ya Wakimbizi waliorejeshwa nchini Burundi kutoka kambi ya Mtabila 
iliyoko Kigoma iliyofungwa rasmi Desemba, 2012 wameingia tena nchini na 
kujazana katika makazi ya muda ya Nyarugusu wakiomba hifadhi.
Kauli
 hiyo imetolewa na Mkuu wa Kambi ya Nyarugusu Sospter Christopher wakati
 akizungumza na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi aliyekwenda kuangalia 
hali halisi ya kambi ya Nyarugusu na Wakimbizi akiambatana na Maofisa wa
 Umoja wa Mataifa akiwemo Mratibu wa Mashirika hayo nchini Alvaro 
Rodriguez.
Kurejea kwa wingi kwa Wakimbizi 
hao ni pigo kisaikolojia kwa watu ambao walirejeshwa nyumbani kwa 
kuonekana kwamba hali ni shwari na walikuwa wameanza kuishi maisha ya 
kawaida.
Mkuu
 huyo wa kambi alisema idadi hiyo ikichanganyika na wengine imafanya  
kambi kuhemewa na kuonekana haja ya kutafuta eneo jingine la kupiga 
kambi kwa ajili ya Wakimbizi hao ambao mpaka mwishoni mwa wiki iliyopita
 walikuwa zaidi ya elfu 51.
“ Kwa sababu tunapokea idadi kubwa
 ya waomba hifadhi toka Burundi, tumekuwa tukiongeza idadi ya vituo vya 
mapokezi ili kukidhi mahitaji ya kuwapokea  wakati tukisubiri maelekezo 
toka ngazi za juu za kuwahamishia Migunga Hills eneo linalopendekezwa 
kufunguliwa kambi ya Nyarugusu B” alisema Christopher mbele ya Waziri 
Chikawe.
Alisema
 walianza kupokea waomba hifadhi hapo kambini kuanzia Aprili 29, 2015 
kwa idadi ndogo kabisa ya watu 36, lakini idadi hiyo ilianza kuongezeka 
siku hadi siku na kufikia Mei 27 mwaka huu idadi yao ilifikia 48,333, 
idadi kubwa ikiwa wanawake na watoto.
Wakimbizi hao walikuwa wakipitia vituo vya Kigoma (27,638), Manyovu (4,439), Kilelema (1,603) na Kigadye (1,291).
Kambi hiyo yenye uwezo wa kubeba 
watu 50,000 imeelemewa kwa sababu ya ujio mpya uliosababisha kuwepo kwa 
Wakimbizi zaidi ya 106,410.
Kuna matatizo zaidi ya milipuko ya
 wagonjwa kambi hii imechanganywa na  Wakimbizi wa Kongo watu ambao 
hawana utamaduni wa pamoja na kuonekana hatari ya kukabiliana kwa 
kutosikilizana.
 Aidha kambi hiyo pamoja na 
kuwahifadhi waburundi wapo pia Wakimbizi kutoka Kongo wapatao 54,706; 
Burundi,3261 ; Rwanda 72; Uganda 17; Sudan Kusini wanane; Kenya 7; 
Somalia 3; Ethiopia 1; Zimbabwe 1; na Ivory coast 1.
Mkurugenzi
 wa Idara ya huduma za Wakimbizi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, 
Harrison Mseke (wa pili kushoto) akizungumza jambo na Mratibu Mkazi wa 
Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo 
(UNDP),  Alvaro Rodriguez (kushoto) huku Mkuu wa kambi mpya 
inayotarajiwa kuanzishwa ya Nyarugusu B, Fredrick Nisajile (wa nne 
kulia) akitoa maelezo kwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mh. Mathias 
Chikawe (wa tatu kushoto) mara tu baada ya kuwasili na kusomewa taarifa 
kwenye kambi ya Nyarugusu wilayani Kasulu mkoani Kigoma. Wengine pichani
 ni baadhi ya viongozi wa ulinzi na usalama wa wilaya ya Kasulu mkoani 
Kigoma.
Akijibu 
 maswali ya waandishi wa habari walioambatana naye katika ziara hiyo 
kuhusu hali ya baadae ya Wakimbizi wa Kongo ambao wapo nchini kwa 
takribani miaka 19 sasa, Waziri Chikawe alisema kwamba serikali haina 
mpango wa kuwapa uraia kwa sasa ingawa Marekani imesema itawachukua 
Wakimbizi elfu 30 kuwapeleka kwao na kwingine duniani.
“hatuna
 mpango wa kuwapa uraia kwa sasa…” alisema Chikawe na kusema kwamba kwa 
kuondolewa kwa hao  wengine kutasaidia kupunguza idadi yao katika kambi 
hiyo.
Alisema
 kwamba ni lengo la serikali kuhakikisha kwamba kambi hiyo inapunguzwa 
ili kuweza kuchangia ipasavyo kwa hali bora ya Wakimbizi na kwamba 
mchakato wa kuwaangalia waomba hifadhi kama wanafaa kuwa Wakimbizi 
unaendelea.
Akizungumzia malalamiko ya 
upatikanaji wa chakula, Waziri Chikawe alisema kwamba si kweli kuwa kuna
 watu hawajapata chakula kwa siku saba la sivyo wangelikufa.
Alisema wengi wa Wakimbizi ni 
watoto na kwamba wanapoingia nchini wanapewa vyakula vikavu (kama 
biskuti)  lakini wakishafika kambini wanapewa chakula kilichopikwa na 
resheni ya siku 14 .
Alisisitiza kuwa kama kungelikuwa hakuna chakula watoto hao wasingeishi, labda kama wanataka kuongezewa chakula zaidi.
Kuhusu
 ujenzi wa kambi mpya Migunga alisema kwamba wataalamu wanaangalia 
barabara mbadala kwani iliyopo sasa pamoja na kuhitajika milioni 300 
kuitengeneza lakini bado kila mvua itakapokuwa inanyesha itahitaji 
kutengenezwa.
Naye
 Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mtaifa la Kuhudumia Wakimbizi 
(UNHCR), Joyce Mends-Cole katika mahojiano na waandishi wa habari 
aliishukuru serikali ya Tanzania kwa kufungua mipaka ili Wakimbizi 
waweze kuingia na kutoa eneo kwa ajili ya kambi mpya kutokana na ya sasa
 kujaa sana.
Aidha aliishukuru serikali ya 
Uingereza kwa kuwa ya kwanza kutoa misaada kwa ajili ya Wakimbizi hao na
 kutarajia nchi nyingine kama Marekani itafanya hivyo mapema ili 
kuisaidia serikali ya Tanzania katika kuhudumia waomba hifadhi.
Naye Mratibu wa Mashirika ya Umoja
 wa Mataifa nchini, Alvaro Rodriguez amesema wanafanya kila 
linalowezekana ili kupunguza idadi ya Wakimbizi katika kambi ya 
Nyarugusu kwa kuwapatia eneo jingine la kujihifadhi.
Alisema kwa kuwatoa hapo 
watasaidia shule zilizofungwa ambazo zinasomesha watoto kutoka kwa 
Wakimbizi wa Kongo kurejea madarasani kukamilisha mtaala wao.
Mkuu wa kambi mpya 
inayotarajiwa kuanzishwa ya Nyarugusu B, Fredrick Nisajile akifafanua 
jambo kwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mh. Mathias Chikawe wakati 
akitembelea na kukagua maeneo mbalimbali ya Kambi ya Nyarugusu iliyopo 
wilayani Kasulu, mkoani Kigoma.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya 
Nchi, Mh. Mathias Chikawe na Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa 
Mataifa, Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), 
Alvaro Rodriguez pamoja na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mtaifa la 
Kuhudumia Wakimbizi (UNHCR), Joyce Mends-Cole wakikagua sehemu 
wanayolala Waomba hifadhi wanaoendelea kuwasili katika kambi ya 
Nyarugusu ambayo inaelemewa kutokana na wingi wa Waomba hifadhi hao 
wanaoendelea kumiminika mjini Kigoma.
Muonekano wa moja ya chumba 
cha kulala familia za waomba hifadhi katika kambi ya Nyarugusu ambapo 
kifika muda wa kulala wanatandika mkeka chini katika vumbi hilo jekundu 
na kupata usingizi.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya 
Nchi, Mh. Mathias Chikawe (mwenye suti ya kijivu), Mratibu Mkazi wa 
Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo 
(UNDP), Alvaro Rodriguez (wa pili kushoto) pamoja na Mwakilishi wa 
Shirika la Umoja wa Mtaifa la Kuhudumia Wakimbizi (UNHCR), Joyce 
Mends-Cole (kushoto) wakisikiliza hoja mbalimbali kutoka kwa Waomba 
hifadhi wanaohifadhiwa kwenye kambi ya Wakimbizi Nyarugusu iliyopo 
 wilaya ya Kasulu mkoani Kigoma walipotembelea kambi hiyo kukagua kambi 
hiyo na kuangalia changamoto mbalimbali zinazowakabili na namna ya 
kuzitatua.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya 
Nchi, Mh. Mathias Chikawe (mwenye suti ya kijivu) akiteta jambo na 
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika 
la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez wakati walipotembelea kambi ya 
Wakimbizi ya Nyarugusu iliyopo wilaya ya Kasulu mkoani Kigoma mwishoni 
mwa juma lililopita.
Waziri
 wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mh. Mathias Chikawe akigawa vifaa vya 
matumizi ya nyumbani ambavyo ni Blangeti, Mkeka, Kontena la kuhifadhi 
chakula na dumu la maji la lita 10 kwa mmoja wa Waomba hifadhi 
waliowasili siku ya ziara ya kutembelea kambi ya Nyarugusu mwishoni mwa 
juma wilayani Kasulu mkoani Kigoma. Anayeshuhudia tukio hilo ni Mratibu 
Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la 
Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez (mwenye shati jeupe).Kulia ni Mkuu wa
 kambi mpya inayotarajiwa kuanzishwa ya Nyarugusu B, Fredrick Nisajile.
Waomba hifadhi  na familia zoa wakiwa katika foleni ya kupokea vifaa hivyo.
Waziri
 wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mh. Mathias Chikawe akizungumza na Waomba 
hifadhi katika kambi ya Nyarugusu wakati alipofanya ziara ya kutembelea 
eneo hilo akiwa ameambatana na Mkuu wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa 
pamoja na Mwakilishi wa shirika la kuhudumia Wakimbizi nchini (UNHCR).
Mtaalam
 wa Mahusiano na Mawasiliano wa Shirika la Umoja wa Mataifa (UN) 
Tanzania, Hoyce Temu akizungumza na mmoja wa wakinamama anayeishi kwenye
 kambi ya Wakimbizi Nyarugusu wakati wa ziara maalum ya kutembelea 
maeneo hayo iliyohusisha Serikali ya Tanzania na Umoja wa Mataifa.
Mratibu
 Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la 
Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez  na Mtaalam wa Mahusiano na 
Mawasiliano wa Shirika la Umoja wa Mataifa (UN) Tanzania, Hoyce Temu 
wakibadilishana mawazo na mmoja wa wafanyakazi wa Shirika la Kimataifa 
Ia Uhamiaji (I.O.M) (katikati) ambaye jina lake halikuweza kupatikana 
kiurahisi katika kambi ya Wakimbizi ya Nyarugusu iliyopo wilayani Kasulu
 mkoani Kigoma.
Mkurugenzi
 wa Idara ya huduma za Wakimbizi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, 
Harrison Mseke (mwenye suti ya kijivu) akifafanua jambo kwa Mh. Mathias 
Chikawe alipotembela katika chumba maalum kichotumika kufanya usajili 
kwa Waomba hifadhi na familia zao kwa ajili ya kupewa hati ya kuwa 
Wakimbizi kamili kama watatimiza vigezo vinavyohitajika. Aliyeketi kulia
 ni Msajili wa Waomba hifadhi, Ndalo Charles Bogohe.
Zoezi la usajili likiendelea kwa familia za waomba hifadhi katika kambi ya Nyarugusu iliyopo wilayani Kasulu mkoani Kigoma.
Wakinamama wakiandaa chakula cha mchana kwa familia zao kama walivyokutwa na kamera ya modewjiblog. 
Sehemu ya familia za Waomba 
hifadhi katika kambi ya Wakimbizi Nyarugusu, wilayani Kasulu, mkoani 
Geita wakiendelea kujipanga baada ya kuwasili kwenye eneo hilo.
Moja ya familia za waomba 
hifadhi ikiwa imejipumzisha mara baada ya chakula cha mchana huku nyuso 
zao zikionekana kuwa na furaha na matumaini mapya.
Hili ni eneo ambalo Waomba hifadhi  kutoka nchini Burundi wa kambi ya Nyarugusu wakiteka maji safi kwa matumizi yao.
Mkurugenzi wa Idara ya huduma 
za Wakimbizi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Harrison Mseke 
(kushoto) akizungumza jambo na Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa 
Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP),  Alvaro Rodriguez 
(wa pili kushoto) wakati wakielekea kukagua vyumba vya madarasa katika 
shule ya msingi Mapendo ambayo yamegeuzwa kuwa nyumba za kulala Waomba 
hifadhi, kutokana na uhaba wa makazi ya kuishi kwenye maeneo ya kambi ya
 Nyarugusu, wilayani Kasulu mkoani Kigoma. Wengine pichani ni baadhi ya 
viongozi wa ulinzi na usalama wa wilaya ya Kasulu mkoani Kigoma katika 
msafara huo.
Baadhi ya Waomba hifadhi 
katika kambi ya Wakimbizi Nyarugusu wakiwa wamempumzika huku wengine 
wakipata chakula cha mchana kama walivyokutwa na kamera ya modewjiblog.
Kinababa nao hushiriki kuandaa chakula cha mchana kwa familia zao kama huyu aliyekutwa na kamera ya modewjiblog.
Eneo
 la shule ya msingi Mapendo katika kambi ya Wakimbizi Nyarugusu ambalo 
kwa sasa linatumika kuhifadhi Waomba hifadhi wanaoendelea kuwasili 
nchini wakitokea Burundi kupitia mji wa Kigoma.
Madawati
 ya wanafunzi katika shule ya msingi Mapendo yakiwa nje ya madarasa 
yakitumika kuanikiwa nguo na huku wakati wa msimu wa mvua yakinyeshewa.
Waziri
 wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mh. Mathias Chikawe na Mratibu Mkazi wa 
Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo 
(UNDP), Alvaro Rodriguez wakibadilishana mawazo na wasimizi wa kambi 
hizo za Nyarugusu wakati wa ziara ya siku moja wilayani Kasulu, mkoani 
Kigoma.
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya 
Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro 
Rodriguez (kushoto) akiwa ameambatana na Waziri wa Mambo ya Ndani ya 
Nchi, Mh. Mathias Chikawe wakikagua eneo jipya litakaloitwa Nyarugusu B 
lililotolewa na serikali kwa ajili ya Waomba hifadhi wanaoendelea 
kumiminika mjini Kigoma ambalo liko mbioni kutengenezwa na kukamilika 
ndani ya miezi 3 ijayo.
Eneo jipya la kambi ya 
Nyarugusu B ambalo limetengwa na serikali ya Jamhuri ya Tanzania kwa 
ajili ya makazi ya Waomba hifadhi wanataotenganishwa Burundi na Congo 
mara tu baada ya kukamilika.
Muonekano
 wa eneo jingine la makazi ya Waombahifadhi ndani ya kambi ya Wakimbizi 
Nyarugusu iliyopo wilayani Kasulu, mkoani Kigoma.
Amani
 na upendo itawale kati yetu……ndivyo wanavyosema kwa pamoja baadhi ya 
watoto waomba hifadhi wakifurahia picha pamoja na Mratibu Mkazi wa 
Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo 
(UNDP), Alvaro Rodriguez.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni