Waziri
 wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo Mh. William Vangimembe Lukuvi akisalimia 
viongozi wa NHC mara baada ya kuwasili eneo la Napupa Masasi kuzindua 
nyumba za gharama nafuu zinazojengwa na NHC. Anayemuongoza Mh. Waziri ni
 Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa NHC Bw. Felix Maagi.
Waziri
 wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo Mh. William Vangimembe Lukuvi akiongea na
 hadhira iliyofurika katika sherehe za uzinduzi wa nyumba za gharama 
nafuu zinazojengwa na NHC Wilayani Masasi.Alizitaka taasisi zinazotoa 
huduma ya umeme na maji kutekeleza majukumu yao ili kupunguza gharama za
 uuzaji wa nyumba zinazojengwa na waendelezaji wote wa makazi.
Sehemu ya umati wa wananchi waliohudhuria sherehe za uzinduzi wa nyumba za gharama nafuu zinazojengwa na NHC Wilayani Masasi.
Kaimu
 Mkurugenzi Mkuu wa NHC Bw. Felix Maagi. Akitoa taarifa ya mradi wa 
nyumba za gharama nafuu zinazojengwa na NHC Wilayani Masasi kwa Waziri 
wa ardhi, nyumba na Maendeleo ya Makazi Mh. William Lukuvi aliyefika 
katika mradi huo wenye nyumba 54 na kuuzindua.
Mkurugenzi
 wa Halmashauri ya Masasi Bi Beatrice Dominic akitoa taarifa ya 
usimamizi wa ardhi kwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo Mh. William 
Vangimembe Lukuvi alipozuru Masasi na kuzindua nyumba za gharama nafuu 
zinazojengwa na NHC.
Waziri
 wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo Mh. William Vangimembe Lukuvi akipewa 
maelezo ya mradi wa nyumba za gharama nafuu zinazojengwa na NHC Wilayani
 Masasi na Kaimu Mkurugenzi wa Uendelezaji Miliki wa NHC Bw. Haikamen 
Mlekio.
Waziri
 wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo Mh. William Vangimembe Lukuvi akiweka 
jiwe la msingi katika nyumba za gharama nafuu zinazojengwa na NHC 
Wilayani Masasi ambazo ujenzi wake utakamilika mwezi Oktoba mwaka huu.
Waziri
 wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo Mh. William Vangimembe Lukuvi 
akisalimiana na wazee aliyowahi kufanya nao kazi Wilayani Masasi mwaka 
1975 akiwa Katibu wa Vijana wa Wilaya, baada ya kukutana nao Ikulu ndogo
 Mjini Masasi.
Waziri
 wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo Mh. William Vangimembe Lukuvi,akionyeshwa
 na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Masasi Bi. Bi Beatrice Dominic mali na 
magari yaliyounguzwa na vijana wa Masasi kutokana na vurugu zilizowahi 
kutokea huko nyuma na kuunguza pia jengo la Ofisi ya ardhi ikiwemo 
nyaraka zote. Hadi sasa Halmashauri hiyo haina Ofisi za kutosha kufanyia
 kazi na wala usafiri wa kusaidia utendaji wa kazi wenye tija.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni