Askari
 wa Jeshi la Zima moto nchini, Josephat John akieleleza matumizi ya 
Kizimamoto wakati wa mafunzo ya menejimenti ya maafa kwa watumishi wa 
Ofisi ya Waziri Mkuu, mjini Dodoma tarehe, 21 Juni, 2015.
Afisa 
Tawala, Ofisi ya Waziri Mkuu, Leah Kibassa, akifanya mazoezi ya kutumia 
kizima moto wakati wa mafunzo ya menejimenti ya maafa kwa watumishi wa 
Ofisi hiyo, mjini Dodoma tarehe, 21 Juni, 2015.
Mkurugenzi
 wa Idara ya Uratibu  Maafa, Ofisi ya Waziri Mkuu, Brig. Jen. Mbazi 
Msuya (mwenye tai) akishuhudia, Salma Juma akikabidhiwa Kizima moto 
kilichonunuliwa na washiriki wa mafunzo ya menejimenti ya maafa wa Ofisi
 hiyo mjini Dodoma tarehe, 21 Juni, 2015,  Kwa lengo la kuhamasisha 
watumishi wa Ofisi hiyo kukabili majanga ya moto.
Watumishi
 wa Ofisi ya Waziri Mkuu wakifuatilia mafunzo ya majanga ya moto  wakati
 wa mafunzo ya menejimenti ya maafa mjini Dodoma tarehe, 21 Juni, 2015.
Na. Mwandishi Maalum
Ofisi ya Waziri Mkuu, Idara ya Uratibu maafa inaandaa mkakati wa elimu kwa umma wa 
menejimenti ya maafa ambao utawatumia watu maarufu nchini wakiwemo wasanii wa 
sanaa mbali mbali  kwa lengo la kufikisha elimu kwa umma ya menejimenti ya maafa. 
Akiongea wakati wa mafunzo ya menejimenti ya maafa kwa watumishi wa Ofisi ya 
Waziri Mkuu, Mjini Dodoma mwishoni mwa wiki hii, Brig.Jen, Mbazi Msuya alibainisha 
kuwa jamii ikielimishwa  kikamilifu  juu ya menejimenti ya maafa athari za maafa 
zinapunguzika.
“Tunaposema menejimenti ya maafa tunazingatia, kuzuia, kukabili  maafa na kurejesha 
hali ya awali baada ya maafa kutokea. Kwa mantiki hii kama  tunavyo elewa Wasanii 
wanao uwezo wa kufikisha ujumbe kwa haraka, lugha nyepesi,  kwa watu  wengi na  
kwa ujumbe mmoja, hili ndo linalotusukuma kufikiria kutumia hawa watu katika kutoa 
elimu ya menejimenti ya maafa kwa jamii yetu” alisema Msuya.
Msuya aliongeza kuwa nchi yetu imekuwa ikikumbwa na majanga ya asili  na yale 
yanayosababishwa na binadamu, ambapo majanga yanayosababishwa na binadamu 
kwa kiwango kikubwa jamii inaweza  kuyakabili  tu ikiwa elimu ya menejimenti ya  
maafa hayo imemfikia kila mwanachi. Hivyo kwa kuwa wasanii wengi msingi wa kazi 
zao za sanaa huaksi yanayojiri katika jamii yao hivyo hii itakuwa ni fursa kwao 
kuijengea jamii uwezo wa kuyakabili maafa.
“Athari za Majanga yanayosababishwa na binadamu kama moto yanaweza kuzuilika 
ikiwa menejimenti ya majanga hayo itatolewa kwa umma. Wananchi wakielimishwa 
umuhimu wa kuwa na vizima moto majumbani mwao na katika vyombo vya moto 
wanaweza kukabili majanga ya moto na hili litawezekana kwani tayari tunayo mikakati 
ya mawasiliano ya kukabiliana na maafa ” alisisitiza Msuya.
Ofisi ya waziri Mkuu kupitia Idara ya Uratibu maafa tayari imeshaandaa  Mkakati wa 
Mawasiliano wa kukabiliana na maafa kwa  mkoa wa Mtwara, Shinyanga na Dodoma 
lengo ikiwa ni kila mkoa nchini kuwa na mkakati huo utakowezesha menejimenti ya 
maafa kwa jamii ya watanzania. Aidha mkakati huo unabainisha kila mdau wa maafa 
wajibu wake katika menejimenti ya maafa wakiwemo wasanii.




Hakuna maoni:
Chapisha Maoni