Mlezi
 wa chama cha wafanyakazi madereva Tanzania (TADWU), Mkuu wa Wilaya ya 
Kinondoni, Paul Makonda (katikati), akizungumza na madereva kabla ya 
kukabidhiwa rasimu ya maboresho ya maslahi ya madereva hao na cheti cha 
utambulisho wa chama hicho Dar es Salaam jana. Kulia ni  Katibu Mkuu wa Chama cha Wafanyakazi Madereva Tanzania (TADWU), Abdallah Lubara na Mwenyekiti wa zamani wa Umoja wa Madereva Tanzania, Clement Masanja.
 Katibu
 Mkuu wa Chama cha Wafanyakazi Madereva Tanzania (TADWU), Abdallah 
Lubara (kulia), akimkabidhi Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda, 
rasimu ya mkataba wa maslahi ya madereva waliyokuwa wakiidai serikali 
kwa muda mrefu Dar es Salaam jana.
Mwenyekiti
 wa zamani wa Umoja wa Madereva Tanzania, Clement Masanja (kushoto), 
akimkabidhi Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda cheti cha 
utambulisho wa chama chao kipya kitakachoitwa Chama cha Wafanyakazi 
Madereva Tanzania (TADWU) baada kuundwa rasmi ambacho kitazindulia Julai
 Mosi mwaka huu.
 Naibu katibu mkuu wa chama hicho, Rashid Said (kulia) akizungumzia yaliyomo kwenye rasimu hiyo na maboresho ya maslahi yao.
 DC Makonda akisalimiana na madereva baada ya kumaliza kwa mkutano huo.
 Madereva wakiwa wamesimama wakisubiri kusalimiana na mlezi wao DC Paul Makonda.
 Ni usikivu kwa mlezi wao wakati akihutubia.
 Mkutano ukiendelea.
 Hapa ni furaha tupu kwa madereva hao.
 Madereva wakiwa kwenye mkutano huo.
 Madereva wakishangilia hutuba ya mlezi wao Paul Makonda.
 Wanahabari kutoka vyombo mbalimbali wakichukua taarifa hiyo.
Mkutano ukiendelea
Na Dotto Mwaibale
CHAMA
 cha Madereva nchini nchini kimemkabidhi mlezi wao Mkuu wa Wlaya ya 
Kinondoni Paul Makonda rasimu ya mkataba uliobeba maboresha ya maslahi 
waliokuwa wanaidai kutoka kwa wamiliki pamoja na Serikali.
Katika
 hatua nyingine madereva hao Julai Mosi mwaka huu wanatarajiwa kuzindua 
chama chao ambacho kitaitwa Chama cha Madereva Wafanyakazi Tanzania 
(TADWU).
Hatua
 ya kutengeneza rasmu hiyo hiyo imekuja baada ya kikao walichokaa Juni 
21 mwaka huu ambapo lengo lilikuwa ni kuwashinikiza waajiri kuwapa 
mikataba ya kudumu wakiwa kazini ikiwa ni pamoja na likizo za uzazi.
Akizungumza
 na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Naibu katibu mkuu wa chama 
hicho, Rashid Said alisema rasimu ya mkataba huo imebeba maboresho ya 
maslahi yao waliyokuwa wanadai.
Alisema
 madai hayo ni pamoja na bima ya maisha , mazishi yenye staha, muda wa 
kazi kisheria, matibabu, na nauli ya kwenda kazini.
"Leo
 tuna chama cha wafanyakazi madereva Tanzania , pia tumepewa mkataba 
hivyo nawatangazia madereva wote kuwa tumepata  chombo cha kuzungumzia 
tofauti na ilivyokuwa awali.
Kwa
 sasa imebaki kujadili na serikali kuhusu kuboreshwa kwa mishahara hivyo
 napenda kuwatangazia madereva kuwa tumepata mikataba tuliyohitaji miaka
 mingi,"alisema.
Katibu
 huyo aliongeza kuwa chama hicho hakitasita kumchulia hatua za kisheria 
mmiliki atakayekiuka sheria hizo na kuongeza hakitasitakumpeleka kwenye 
vyombo vya sheria kama walivyokuwa wanawafanyia mwanzoni.
Akikabidhiwa
 mkataba huo kwa chama hicho, Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda 
alisema mahali walipofikia madereva hao kwa sasa ni jambo la kuleta 
maendele makubwa.
Alisema
 watanzania wanatakiwa kutambua kuwa madai hayo si kwa ajili ya madereva
 peke yao  bali ni kwa ajili ya taifa zima na kwamba kutatuliwa kwa 
changamoto hiyo kutapunguza ajali zinazoendelea kutokea nchini.
Makonda
 alisema asilimia kubwa ya madereva wamekuwa wakipata ajali kutokana na 
kuchoka hivyo wanaposinzia usahau kuwa wanaendesha vyombo vya moto hivyo
 kusababisha ajali.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni