MAADHIMISHO YA SIKU YA WATU WENYE UALBINO YAFANA JIJINI ARUSHA JANA ,RAIS KIKWETE AKEMEA IMANI POTOFU

Mkurugenzi Mkazi waUmoja wa Mataifa(UN)Alvaro Rodriguez akihutubia katika Maadhimisho ya Siku ya wenye Ualbino yaliyofanyika  kwenye uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha.

Mkurugenzi Mkazi waUmoja wa Mataifa(UN)Alvaro Rodriguez akihutubia katika Maadhimisho ya Siku ya wenye Ualbino yaliyofanyika  kwenye uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha.

Mkurugenzi Mkazi waUmoja wa Mataifa(UN)Alvaro Rodriguez akipongezwa na Rais Jakaya Kikwete baada ya kutoa hotuba yake  katika Maadhimisho ya Siku ya wenye Ualbino yaliyofanyika  kwenye uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha.

Balozi wa Canada hapa nchini,Alexandre Leveque akihutubia katika Maadhimisho ya Siku ya wenye Ualbino yaliyofanyika kwenye uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha.

Mwenyekiti wa wenye ulemavu wa ngozi nchini(TAS)Ernest Kimaya akitoa nasaha zake.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dk Jakaya Kikwete akihutubia wananchi waliohudhiria maadhimisho hayo kwenye uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha.Alitumia fursa hiyo kukemea mauaji yanayofanywa na dhidi ya Albino kwa imani za kishirikina.

Naibu Waziri wa Afya,Dk Kebwe Stiven Kebwa akitoa nasaha zake.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dk Jakaya Kikwete akiwapongeza watoto wenye Ualbino wanaofadhiliwa na USAID chini ya mpango wa Pamoja Tuwalee.


Baadhi ya watu wenye ulemavu wakiwa kwenye maandamano .

Baadhi ya watu wenye ulemavu wakiwa kwenye maandamano .


Baadhi ya watu wenye ulemavu wakipita na mabango yenye ujumbe katika mitaa mbalimbali ya Jiji la Arusha kwa  maandamano kwenye maadhimisho ya Siku yao ambayo inalenga kutoa elimu ya kupinga matendo maovu wanayofanyiwa na watu wenye nia mbaya.

Baadhi ya watu wenye ulemavu wakiwa kwenye maandamano.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dk Jakaya Kikwete akiagana na Balozi wa Canada hapa nchini,Alexandre Leveque baada ya maadhimisho hayo,kulia ni Mkurugenzi Mkazi wa Umoja wa Mataifa(UN) hapa nchini,Alvaro Rodriguez na Mkuu wa Mkoa wa Arusha,Felix Ntibenda.




Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania ameonyesha kusononeshwa na mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi yanayoendelea nchini kwenye uso wa sura za kimataifa.

Rais Kikwete aliyasema hayo jana kwenye kilele cha maadhimisho ya watu wenye Ualbino  kuongeza uelewa juu ya watu wenye ualbino pamoja na kupinga unyanyapaa, unyanyasaji na mauaji ya Albino yaliyofanyika duniani kote mkoani Arusha mapema jana katika viwanja vya sheik amri abeid.

Rais Kikwete alisema kuwa matukio ya mauaji na ukataji viungo vya Albino imekuwa fedheha kwake hasa anapotembelea nchi zingine .


“Naomba niseme kuwa imani hizi za kusema eti kuwa kiungo cha binadamu mwenzako inaweza kusababisha utajiri au kupata cheo hizi ni za kupiga vita kabisa kwani kila mtu anajua kabisa chanzo cha mafaniki yoyote au utajiri ni kufanya kazi kwa bidii, juhudi na ufanisi kazini” alisema Rais Kikwete.

Akijibu juu ya ucheleweshaji wa utekelezaji wa kesi za mauaji, Rais Kikwete alisema kuwa jumla ya watu 139 wamekamatwa na 15 wamepatikana na hatia ambapo 13 kati yao wamehukumiwa kunyongwa lakini bado hawajanyongwa kutokana na msururu wa hatua za kupitisha zoezi hilo kukamilika hivyo wavute subira kwani linafanyiwa kazi.

“Katika msako ule tuliyoendesha kuanzia mwaka 2006 hadi2010 juu ya matukio haya, tulifanikiwa kukamata watu 139 ambapo walipelekwa mahakamani na baadae watu 15 wakakutwa na hatia hivyo wawili kati yao wakapewa adhabu ya kawaida na 13 wakahukumiwa kunyongwa huku wengine wakiachiwa kwa kuonekana hawana hatia”

“Lakini naomba niseme ndugu zangu kuwa kesi za mauaji si kesi ndogo hivyo huendeshwa kwa mda mrefu ili kujiridhisha kuwa anaenyongwa ndie muhusika halisi wa kosa isije kutokea akanyongwa mtu asiyehusika hivyo kuna mlolongo mrefu sana wa kesi hizo hivyo tuvumiliane tu maana watu wawili karibu msururu wao unaisha na adhabu zitatolewa”


Akizungumzia swala hili, Rais Kikwete alionekana kama anampigia debe Waziri wa mambo ya ndani Mathias Chikawe baada ya kusema kuwa waziri huyo kwakuwa ametangaza nia ya kugombea urais, endapo atapata basi swala hili litakuwa limefika sehemu salama.

Waziri Chikawe ebu njoo useme kidogo swala la mapambano ya albino lilipofikia kwani naona pia umevuta fomu ya kugombea Urais na kama utapata naamini swala hili litamalizika haraka, hivyo jamani kama akipata kuwa Rais wanchi. 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni