  | 
| Christian Bella akijimwaga jukwaani. | 
Masaa 
machache baada ya kukosa kitatanishi tunzo ya wimbo bora wa mwaka katika
 Kili Music Awards Christian Bela (King of melodies) alipagawisha 
wapenzi wa muziki mjini Tabora alipoporomosha bonge la show akiwa na 
kundi zima la Malaika Band. Christian Bela alitarajiwa na  wadau wa 
muziki nchini kuwa angebeba tunzo hiyo bila ushindani mkubwa kutokana na
 wimbo wake wa Nani kama mama ambao aliomshirikisha Ommy Dimpoz kutamba 
sana katika vituo vyote vya redio na Runinga hapa nchini, lakini kama 
kawaida ya tunzo hizo zinazosimamiwa na BASATA na kudhaminiwa na kampuni
 ya utengenezaji bia ya Tanzania TBL zimekuwa zikilalamikiwa kila mwaka 
huku waanadaaji wakioneka kuweka pamba mbichi masikioni. Tunzo hiyo ya 
wimbo bora wa mwaka ilienda kwa wimbo wa Mwana wa msanii Ali Kiba. 
Onesho hilo lilifanyika katika viwanja vya Bwalo la Polisi Tabora.
  | 
| Bella akifanya yake jukwaani. | 
  | 
| Mashabiki wa Malaika Band wakpozi | 
  | 
| Hapo sasa! | 
  | 
| Baadhi ya mashabiki wakijmwaga! | 
  | 
| Music Producer Dula K kulia na msanii Masha Kay kushoto wakiwa na mdau. | 
  | 
| Wacha wee Benny Ngwasuma akijiachia | 
Picha na habari na Mkala Fundikira TBN CENTRAL ZONE
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni