CHAMA CHA MAPINDUZI WILAYA YA ARUSHA CHATOA ONYO

Mahmoud Ahmad Arusha
KATIBU wa chama cha Mapinduzi wilaya ya Arusha , Feruzi Banno amewataka watiania ya kuomba ridhaa ya Ubunge kupitia chama cha mapinduzi  jimbo la Arusha , kuacha kampeni kabla ya wakati .

Onyo hilo amelitoa jana alipokuwa akizungumza na watia nia kumi na mbili kati ya kumi na nane walioonyesha nia ya kugombea ubunge kupitia CCM.

Katibu Feruzi, amewaambia watia nia hao kuwa Chama cha mapinduzi kina kanuni na maadili ambayo kila mtia nia anapaswa kuyazingatia ili kuepuka asipoteze sifa ya kuwa miongoni mwa wagombea watakaopitishwa na chama .

“NInawakumbusha kila mmoja wenu kuzoifuata na kuzizingatia kanuni hizo na atakae kiuka atachukuliwa hatua ikiwa ni pamoja na kuondolewa kwa kuwa amepoteza sifa’’,alisema Feruzi.

Alisema kuwa chama kimeshapokea taarifa za kuwepo kwa baadhi ya wagombea kuanbza kampeni kabla ya wakati na hilo likithibitika wataondolewa.

Aliwataka watia nia wote kutokuchafuana  wa kupakana matope bali wazingatie taratibu.Akijibu maswali ya wanahabari kuwepo taarifa za baadhi ya wagombea kuchapisha Tsheti na Vipeperushi ,Katibu, alisema chama kinafuatilia nyendo za watia nia hao na ikibainika watachukuliwa hatua.

Banno ,alisisitiza   kanuni na maadili ya uongozi katika uchaguzi ndani ya chama hicho yanatakiwa kufuatwa na kila mtia nia na kuwa atakayekiuka kanuni na taratibu  za chama  kwa kuanza kampeni mapema chama kitafuata kanuni na taratibu za uchaguzi ndani ya chama kumwajibisha.

Alisema kuwa Form ndani ya chama hicho zitaanza kutolewa June 15 na mwisho wa kurudisha form za kuomba ridhaa ya ubunge ndani ya ccm ni June 19 saa kumi jioni na  kura za maoni zitafanyika August 1 na kuwataka atakayepitishwa kumuunga mkono kwa nguvu zao ilikuweza kulirudisha jimbo kwenye mikono ya chama hicho.

Amewataka watia nia hao Kimu Fute,David Rwenyagira,Justin Nyari,Philemon Mollel,Aziz Nassoro,Deo Mtui,Edmund Ngemela,Mahmoud Said,Michael Sekajingo,Victor Njau,Mustaf Panju na Aloice Kilimbo wawe na umoja, mshikamano na upendo na wawe tayari kukabali matokeo na kumuunga mkono mgombea ambae atakuwa ameshinda.

Ametoa wito kwa wanachama wengine wa ccm, wenye nia ya kugombea ubunge katika jimbo hilo kujitokeza kwa wingi .Wakizungumza kwa nyakati tofauti mara baada ya kikao hicho watia nia hao wamesema wameridhishwa na hatua ya katibu kuwakutanisha na hivyo kufahamiana.

Akizungumzia hatua hiyo, mgombea mmoja David Rwenyagira,
amesema utaratibu uliowekwa na chama ni mzuri hivyo kila mgombea anapaswa kuuheshimu.Kwa upande wake Kim Fute, amepongeza hatua hiyo na kuahidi kufuata taratibu na kanuni za ccm.

Kwa upande wake Justin Nyari, yeye ameahidi kuzingatia kanuni na taratibu .

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni