GOLA KUWAONDOA WATOTO WA MITAANI JIJINI ARUSHA

Mkurugenzi wa shirika lisilokua la kiserikali la Gola Foundation ,Elisha Maghembe amesema kuwa wameanza zoezi la  kuwaondoa watoto wa mitaani walioko  jijini Arusha na kuwafikisha kwenye vituo maalumu vya malezi lengo ikiwa ni kuwarudisha makwao pamoja na kuwapatia fursa ya elimu waliyoikosa kwa muda mrefu.

Elisha alisema kuwa zoezi hilo limeanza mapema mwaka huu ambapo mpaka sasa wamewakusanya watoto 25 na kuwapeleka katika kituo chao cha malezi kilichopo wilaya ya Arumeru ambapo watoto watano walitambuliwa na kuchukuliwa na wazazi wao.

Amesema kuwa watoto wa mitaani wanapokaa mtaani kwa muda mrefu hujitumbukiza katika majanga ya matumizi ya madawa ya kulevya na kufanya vitendo visivyofaa hivyo ameitaka jamii ishirikiane kutatua tatizo hili ambalo ni janga kwa taifa.

“Tunapofika mtaani kuwaondoa watoto hawa wa mtaani tunakutana na changamoto nyingi ikiwemo kukosa ushirikiano na watoto wenyewe na pia wengine wanatumkishwa na ajira katika umri mdogo na baadhi ya watu hivyo kufanya zoezi hilo kuwa gumu” Alisha Elisha

Afisa ustawi wa jamii na Maendeleo ya jamii jijini A Mwantumu Dossi  alifika katika kituo cha kufikia cha malezi ya watoto wa mtaani kinachomilikiwa na Gola Foundation amesema kuwa Halmashauri ya jiji itaangalia namna ya kushirikiana kutatua changamoto za watoto wa mitaani.

“Tatizo la watoto wa mitaani ni tatizo sugu nimefika apa kujionea na kama Jiji kuna mkakati Mahususi wa kuwaondoa watoto wa mitaani utakaoanza 2015-2016” alisema Mwantumu

Mwenyekiti wa Baraza la watoto wilaya ya Arusha Hassan Omari alisema kuwa juhudi za kuwaondoa watoto wa mitaani katika mazingira magumu na hatarishi zinapaswa kuungwa mkono na kila mtu pamoja na serikali kwani watoto ni taifa linalotegemewa kesho.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni