Na Mwandishi Wetu 
 KAMPUNI
 ya Simu Tanzania (TTCL) imekabidhi mradi wa kuiunganisha matawi 12 ya 
Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) katika huduma za mawasiliano ya sauti, 
intaneti pamoja na data ili kuviwezesha vituo hivyo kufanya kazi katika 
mfumo wa kisasa kimawasiliano jambo ambalo litaboresha utendaji kazi wa 
kampuni hiyo. 
 Akikabidhi
 mradi huo leo jijini Dar es Salaam, Ofisa Mkuu wa Masoko na Mauzo wa 
kampuni ya TTCL, Peter Ngota alisema kwa sasa wamekamilisha kuyaunga 
kimawasiliano ya kisasa matawi 12 ya kampuni ya bia Tanzania ambayo ni 
pamoja na tawi kuu la Dar es salaam (HQ), Arusha, Moshi, Mwanza, Ubungo,
 Mwenge, Konyagi, Masaki, Bukoba, Shinyanga, Iringa na tawi la Tanga. 
 Alisema
 mfumo huo wa mawasiliano unaunganisha makao makuu ya ofisi na matawi 
yake ambayo yako maeneo tofauti nchini kwa lengo la kurahisisha utoaji 
na upokeaji wa Taarifa 
(Data) huku ukiwa salama tofauti na mifumo mingine. 
 "...Katika
 mfumo huu wa Multiprotocol Label Switching Virtual Private Network 
(MPLS VPN), Tanzania Breweries Ltd inapata huduma ya sauti, intaneti 
pamoja na data. Kwa huduma hizi TBL sasa iendelee kwa kasi kuboresha 
mifumo ambayo itasaidia kuongeza tija katika utendaji kazi wake na kwa 
wateja kwa ujumla," alisema Ngota.
Ofisa huyo Mkuu wa Masoko na Mauzo aliongeza kuwa kwa sasa TTCL ni 
kampuni pekee yenye mtandao wa Mkongo (Fibre) ambao umesambaa nchi nzima
 huku ukiwa chachu ya kuleta mabadiliko katika kutoa huduma kwa wananchi
 na utendaji kazi wa jumla wa makampuni mbalimbali. 
 TTCL 
imekuwa nguzo muhimu kwa Taasisi za kifedha (Kibenki), Balozi, 
Mashirika, Wizara na taasisi za serikali, makampuni ya kimataifa na 
binafsi katika kuboresha utendaji na uendeshaji wa shughuli zao 
kisayansi na kukidhi viwango vya kimataifa. 
TTCL 
pia imefanikiwa kuunganisha wateja mbalimbali ikiwa ni pamoja taasisi na
 ofisi za serikali; TAMISEMI, Wizara ya Afya, Wizara ya Elimu na Mafunzo
 ya Ufundi, Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Wizara
 ya Fedha, Kampuniya Mapato Tanzania (TRA), Shirika la Bima la Taifa 
(NIC). 
 Alisema
 huduma hiyo ya mkongo pia imerahisisha kazi katika Hospitali ya 
Muhimbili, Mwananyamala, Temeke, MOI, Bugando, KCMC pamoja na Hospitali 
za Mkoa nchi nzima ikiwemo Zanzibar pia zinaendelea kuunganishwa kupitia
 Mkongo wa TTCL kwa huduma bora za kiafya kupitia afya mtandao.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Fedha wa Kampuni ya TBL, Kevin O'Flaherty 
akipokea mradi huo alisema tayari wameanza kuona mafanikio makubwa baada
 ya kuanza kutumia mfumo huo huku ukisaidia kukua kwa biashara yao 
tofauti na awali. 
 Aidha
 alisema kutokana na mabadiliko ya sayansi na teknolojia yanayoendelea 
kukua kila uchao kampuni hazina budi kufanya kazi kwa kutumia teknolojia
 mbalimbali ili kuongeza ufanisi wa kazi na ubora hali itakayochangia 
kukua pia kwa biashara zao. "...Tayari tumeanza kuona mafanikio tangu 
kuanza kutumia huduma hii na tunaamini tutapata mafanikio zaidi, kwa 
sasa unaweza kutofautisha na ilivyokuwa kabla ya kuanza kutumia MPLS 
VPN," alisema O'Flaherty.*
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni