Erick Evarist
 OHOOO! 
Mchekeshaji maarufu Bongo, Steven Mengere ‘Steve Nyerere’ amedaiwa 
kupewa fedha za kampeni kutoka kwa wagombea wawili tofauti wa urais 
2015, Bernard Membe na Stephen Wasira.
Chanzo makini kimepenyeza ubuyu kuwa, Steve hakuwa na msimamo wa 
kumfanyia kampeni mgombea mmoja kwani Jumamosi iliyopita alilipwa na 
kwenda mkoani Mwanza…
                                 
Erick Evarist
 OHOOO! 
Mchekeshaji maarufu Bongo, Steven Mengere ‘Steve Nyerere’ amedaiwa 
kupewa fedha za kampeni kutoka kwa wagombea wawili tofauti wa urais 
2015, Bernard Membe na Stephen Wasira.
Chanzo makini kimepenyeza ubuyu kuwa, Steve hakuwa na msimamo wa 
kumfanyia kampeni mgombea mmoja kwani Jumamosi iliyopita alilipwa na 
kwenda mkoani Mwanza kumuunga mkono Wasira alipokuwa anatangaza nia huku
 pia akiwa ameweka kibindoni ‘mtonyo’ wa Membe.
“Jamaa amekula huku na huku. Jumamosi iliyopita aliwachukua wenzake 
kina JB (Jacob Steven) na Ray (Vincent Kigosi) wakaenda Mwanza kwa 
Wasira kumuunga mkono alipokuwa anatangaza nia. Wakati huohuo amelamba 
mkwanja wa Membe ambapo Jumamosi hii (leo) anatarajia kwenda kumuunga 
mkono nyumbani kwake Mtama atakapokuwa anatangaza nia,” kilisema chanzo 
chetu.
Mwanahabari wetu alimtafuta Steve Nyerere ili kumsikia anazungumziaje
 suala la yeye kudaiwa kufanya kampeni kwa wagombea wawili tofauti 
wakati inaaminika kabisa msikie alichojibu:
“Watu wanashindwa kuelewa, Wasira aliniita mimi na wenzangu kama 
rafiki na si kazi. Bila hiyana tuliamua kwenda na ndiyo maana pale 
hutukuzungumza sababu tulikuwa kama waalikwa wengine.“Kwa Membe hiyo 
haina kificho, nitakwenda na wenzangu kama kazi sababu ni kweli namuunga
 mkono kitambo tu, si leo wala jana,” alisema Steve Nyerere.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni