STEVE NYERERE ADAIWA ‘KULA’ KWA MEMBE, WASIRA

Mchekeshaji maarufu Bongo, Steven Mengere ‘Steve Nyerere’.
Erick Evarist

OHOOO! Mchekeshaji maarufu Bongo, Steven Mengere ‘Steve Nyerere’ amedaiwa kupewa fedha za kampeni kutoka kwa wagombea wawili tofauti wa urais 2015, Bernard Membe na Stephen Wasira.
Steve Nyerere akifafanua jambo kuhusiana na siasa pamoja na filamu.
Chanzo makini kimepenyeza ubuyu kuwa, Steve hakuwa na msimamo wa kumfanyia kampeni mgombea mmoja kwani Jumamosi iliyopita alilipwa na kwenda mkoani Mwanza…
Mchekeshaji maarufu Bongo, Steven Mengere ‘Steve Nyerere’.
Erick Evarist
OHOOO! Mchekeshaji maarufu Bongo, Steven Mengere ‘Steve Nyerere’ amedaiwa kupewa fedha za kampeni kutoka kwa wagombea wawili tofauti wa urais 2015, Bernard Membe na Stephen Wasira.
Steve Nyerere akifafanua jambo kuhusiana na siasa pamoja na filamu.
Chanzo makini kimepenyeza ubuyu kuwa, Steve hakuwa na msimamo wa kumfanyia kampeni mgombea mmoja kwani Jumamosi iliyopita alilipwa na kwenda mkoani Mwanza kumuunga mkono Wasira alipokuwa anatangaza nia huku pia akiwa ameweka kibindoni ‘mtonyo’ wa Membe.
“Jamaa amekula huku na huku. Jumamosi iliyopita aliwachukua wenzake kina JB (Jacob Steven) na Ray (Vincent Kigosi) wakaenda Mwanza kwa Wasira kumuunga mkono alipokuwa anatangaza nia. Wakati huohuo amelamba mkwanja wa Membe ambapo Jumamosi hii (leo) anatarajia kwenda kumuunga mkono nyumbani kwake Mtama atakapokuwa anatangaza nia,” kilisema chanzo chetu.
Mwanahabari wetu alimtafuta Steve Nyerere ili kumsikia anazungumziaje suala la yeye kudaiwa kufanya kampeni kwa wagombea wawili tofauti wakati inaaminika kabisa msikie alichojibu:
“Watu wanashindwa kuelewa, Wasira aliniita mimi na wenzangu kama rafiki na si kazi. Bila hiyana tuliamua kwenda na ndiyo maana pale hutukuzungumza sababu tulikuwa kama waalikwa wengine.“Kwa Membe hiyo haina kificho, nitakwenda na wenzangu kama kazi sababu ni kweli namuunga mkono kitambo tu, si leo wala jana,” alisema Steve Nyerere.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni