TANAPA YAKUTANA NA WAHARIRI WA VYOMBO VYA HABARI NCHINI JIJINI MWANZA KUKUZA UTALII

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Hifadhi za Taifa nchini(Tanapa)Allan Kijazi akifungua Kongamano la Wahariri wa vyombo mbalimbali vya Habari nchini lenye kauli mbiu “Wajibu wa Vyombo vya habari katika kukuza Utalii”inayofanyika katika hoteli ya Gold Crest jijini Mwanza.

Baadhi ya watumishi wa Tanapa wakiwa na Wahariri wa vyombo mbalimbali vya Habari wakifatilia kwa makini hotuba ya Mkurugenzi Mkuu wa Tanapa.

Waandishi Adam Ihucha(The East African)Paul Sarwat(Raia Mwema)na Charles Ngereza(Radio One) wakiwa miongoni mwa waandishi waandamizi wanaoshiriki Kongamano hilo jijini Mwanza.

Wahariri wa vyombo vya habari nchini wakiwa kwenye Kongamano lililoandaliwa na Tanapa kwaajili ya kuwapa uelewa wa mambo mbalimbali yanayolihusu shirika hilo lenye jukumu la kuhifadhi na kukuza utalii nchini.

Wahariri wa vyombo vya habari na Waandishi wa habari Waandamizi  nchini wakiwa kwenye Kongamano lililoandaliwa na Tanapa kwaajili ya kuwapa uelewa wa mambo mbalimbali yanayolihusu shirika hilo lenye jukumu la kuhifadhi na kukuza utalii nchini.

Baadhi ya watumishi wa Tanapa wakiwa na Wahariri wa vyombo mbalimbali vya Habari wakifatilia kwa makini hotuba ya Mkurugenzi Mkuu wa Tanapa.

Wahariri wakibadilisha na mawazo



SALAM ZA MKURUGENZI MKUU WA SHIRIKA LA HIFADHI ZA TAIFA
NDUGU ALLAN KIJAZI KATIKA UFUNGUZI WA WARSHA YA
WAHARIRI WA HABARI TANZANIA, MWANZA, 29.06.2015
·        Ndugu Wahariri wa Habari kutoka vyombo mbalimbali nchini;
·        Ndugu waandishi wa habari
·        Menejimenti ya TANAPA
·        Mabibi na Mabwana;
Napenda kuchukua fursa hii kutoa shukrani zangu za dhati kwenu Wahariri kutoka Vyombo mbalimbali vya habari nchini kwa kukubali mwaliko wetu wa kuhudhuria Warsha hii nina imani kwamba munaelewa umuhimu wa uhifadhi na sekta ya Utalii kwa maendeleo ya nchi yetu. Tunaelewa bayana majukumu mazito mliyo nayo, lakini kwa heshima kubwa mmekubali kutenga muda wenu kujumuika nasi. Tunawashukuru sana kwa moyo huo.  TANAPA tutaendelea kuthamini ushirikiano huu mnaoendelea kutuonyesha siku hadi siku.
Ndugu Wahariri na Waandishi wa Habari,
Utalii ni sekta mtambuka na inachochea ukuaji wa sekta nyingine ikiwa ni pamoja na kilimo, usafirishaji wa anga na barabara, huduma za fedha, huduma za chakula na malazi kudorora kwa sekta nyingineazi.  Hivyo kudorora kwa sekta hii huchangia kwa kiasi kikubwa kudorora kwa sekta nyingine.  Aidha, hadi sasa, Utalii unaongoza katika kuingiza fedha za kigeni ikiwa ya kwanza na kufuatiwa na sekta ya madini na kilimo.  Kwa  na kwa ujumla unachangia asilimia 17.5 ya Pato la Taifa lakini tathmini inaonyesha sekta hii inaweza ikachangia zaidi ya 30% ya pato la Taifa.  Asilimia zaidi ya 80 ya utalii nchini ni utalii wa kutembelea kwenye Hifadhi za Taifa, na hii inaonyesha kuwa hifadhi hizi ni muhimu kwa ustawi wa taifa letu.  Ni zaidi ya mara tatu ya idadi ya wanaotembelea Hifadhi hizi.
Ndugu Wahariri,
Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) linayo dhamana ya kusimamia maeneo yote yaliyotengwa kisheria kama Hifadhi za Taifa nchini. Dhamana hii tuliyopewa na nchi ni kubwa inayohitaji ushirikishwaji wa wadau mbalimbali. Hivyo,TANAPA imekuwa ikijitahidi sana kuinua uhifadhi katika maeneo mengi tuliyokabidhiwa na Serikali. Mfano wa maeneo hayo ni Saadani, Mkomazi na Kitulo. Maeneo haya yalikuwa na hali mbaya sana ya kiuhifadhi kabla hayajakabidhiwa kwa TANAPA, lakini kwa sasa maeneo hayo ni mazuri na yanaanza kuvuvutia wageni na idadi ya wanyama inaongezeka hasa katika Hifadhi za Saadani na Mkomazi.
Ndugu Wanahabari,
Maeneo yaliyo chini ya Hifadhi za Taifa yana faida nyingi za kiikolojia (ecosystem services) kama vile kuwa vyanzo vya maji (mfano; Hifadhi za Kilimanjaro, Arusha na Udzungwa). Maji hayo pia hutumiwa kwa ajili ya kuzalisha umeme unaotumika kwenye gridi ya Taifa. Hivyo faida za kusimamia Hifadhi hizi haziishii tu kwa watalii kufurahia bali pia kuna faida nyingine za kiuchumi ambazo sio rahisi sana kuziainisha katika mfumo wa kifedha (i.e. other values which are not easily tagged in financial terms).
Mabibi na Mabwana,
Takribani fedha zote  za uendeshaji wa Shirika zinatokana na shughuli za utalii.  Hivyo,ili tufanikiwe tumekuwa tukitangaza vivutio vyetu ndani na nje ya nchi. Juhudi hizi zimetuwezesha kufanya vizuri katika soko na kupata Tuzo mbalimbali kimataifa.
Kwa mwaka huu tu wa 2015, mtandao maarufu kimataifa unaojulikana kwa jina la Safari Bookings” uliiteua Hifadhi ya Taifa ya Serengeti kuwa “The best park for African safaris” na hii ni baada ya kushindanishwa na hifadhi nyingine 50 Barani Afrika zikiwemo za Afrika Kusini.
Aidha, Hifadhi za Mikumi na Arusha zilitunukiwa “Certificate of Excellence” na mtandao maarufu duniani ujulikanao kama TripAdvisor. Vilevile, tumekuwa tukipata tuzo mbalimbali kwa ushiriki wetu kwenye maonyesho ya kimataifa na Mwezi Juni mwaka huu Banda la TANAPA kwenye maonyesho ya Korea World Travel Fair lilipata “The Best Tourism Marketing Award”. Nitumie fursa hii kutoa shukrani kwa wadau wote tulioshirikiana kwa njia moja au nyingine katika kupata tuzo hizi.
Ndugu Wahariri,
Hifadhi ya Serengeti imepata jumla ya alama 4.89 kati ya 5-98%.  Kwa mara ya kwanza Hifadhi ya Ruaha imeingia kwenye kumi bora kama best park for African safaris.  Katika vivutio 140 vilivyoshindanishwa zipo hifadhi za Taifa nne ambazo zimeingia kwenye vivutio hamsini bora.  Hifadhi hizo ni Serengeti, Ruaha, Katavi (22) na Tarangire (42).
Mwelekeo huu mpya wa kuendelea kutambulika kwa Hifadhi kati ya ukanda wa kusini na kaskazini mwa Tanzania.  Hali hii ni muhimu kwa uwiano wa maendeleo (balanced dev.)  Tunashukuru wadau wote, hasa vyombo vya habari kwa jitihada kubwa zilizofanyika kuvitangaza vivutio vyetu.
Pamoja na mafanikio haya, hatuna budi kuongeza weledi na kasi ya kuvitangaza vivutio vyetu ili viingie kwa wingi zaidi kwenye orodha ya vivutio bora vya Afrika.
Tunategemea pia kwamba jitihada hizo zitajikita kwenye kupambana na ujangili ambao umebadilika sura kila mara, kwani unatishia uwepo wa rasilimali zetu ambazo ni urithi wa kizazi hiki na vzazi vijavvyo.
Ndugu wanahabri,
Tusiposhikamana na kushinda vita dhidi ya ujangili, tutakuwa tumewakosea haki Watanzania.
Ushirikishwaji wa vyombo vya habari umekuwa unatekelezwa na TANAPA kwa njia mbalimbali ikiwa ni pamoja na kukutana na Wahariri na Wanahabari mbalimbali kila mwaka, kufanya ziara mbalimbali zinazojumuisha vyombo vya habari katika maeneo yetu ya Hifadhi za Taifa; pamoja na kuwa na vipindi katika vyombo mbalimbali vya habari tukilenga kuifahamisha jamii shughuli zetu pamoja na wajibu wa sekta nyingine katika kuunga mkono shughuli za uhifadhi na utalii.
Mkutano huu wa Mwanza unakuwa ni wa tatu kuwahusisha Wahariri na Wahariri wa Habari ambao kimsingi ndio wasimamizi muhimu katika utoaji wa habari kila siku katika vyombo wanavyotoka. Mwaka jana Mkutano kama huu ulifanyika hapa hapa Mwanza. Mikutano hii imekuwa na mafanikio makubwa sana kwa Shirika na hasa tunaona kuwa kiwango na mwamko wa wanahabari kuandika masuala ya uhifadhi na utalii hususan katika Hifadhi za Taifa unakua kwa kiwango kikubwa.
Ndugu Wanahabari,  
Eneo la Utalii wa Ndani nalo limekuwa ni changamoto kubwa sana kwa shirika ambapo licha ya sekta utalii hii kuwa na fursa kubwa kutoa mchango mkubwa kwenye uchumi wa nchi, bado kwa kiwango kikubwa tumekuwa tukitegemea wageni kutoka nje ya nchi. Ni dhahiri kuwa wakati umefika sasa kwa Watanzania kujenga utamaduni wa kutembelea maeneo haya kwa ajili ya kutalii. TANAPA kwa upande wake itatoa ushirikiano katika kufanikisha dhamira kwa mustakabali mzuri wa uchumi wa nchi yetu.
Kauli mbiu ya Mkutano wa mwaka huu ni  “Wajibu wa Vyombo vya Habari katika kukuza utalii”. Pamoja na kuelezea shughuli za TANAPA, mada zitakazowasilishwa zitahusu masuala ya Utalii na Uhifadhi na namna wanahabari wanavyoweza kushirikiana nasi katika kuhimiza uhifadhi na kuendeleza utalii.  Mada kuu nne zitawasilishwa na viongozi wa TANAPA na wanazuoni maarufu akiwemo Nd. Jenerali Ulimwengu na Dkt. Alfred Kikoti. Inatarajiwa kuwa washiriki watapata fursa ya kuchangia na mwishoni watatushauri namna ya kuboresha utekelezaji wa majukumu yetu.
Ndugu Wahariri,
Baada ya kusema hayo, naomba sasa nitamke kuwa warsha hii imefunguliwa rasmi na niwaombe mchangie na kutoa ushauri na maoni mazuri yatakayotusaidia sote kwa pamoja kuendeleza sekta ya uhifadhi na utalii nchini.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni