Mamia ya Waakazi wa Mji wa Bukoba na Vitongoji vyake wakiwemo na Wageni mbalimbali kutoka nje ya Mkoa huu na nje ya Nchi wamejitokeza kwa wingi kumzika marehemu Samuel Luangisa leo Jumatano juni 3, 2015 nyumbani kwake Kitendaguro nje kidogo na Mji wa Bukoba. Marehemu Samuel Luangisa ni miongoni mwa waasisi wa Taifa na katika vipindi tofauti alikuwa Mkuu wa Mkoa wa Ziwa Magharibi(Kagera) Mbunge na Meya wa Manispaa ya Bukoba pamoja na nyadhifa nyingine.
Mbunge wa muleba kusini Prof Anna Kajumulo Tibaijuka
Taswira za picha enzi ya uhai wa Marehemu Mhe. Samuel Luangisa
Merehemu
 Samwel Lwangisa alizaliwa mwaka 1932 na mauti yalimkuta New York 
Marekani tarehe 25.05.2015 na kuzikwa leo Jumatano juni 3, 2015 Nyumbani
 kwake Kitendaguro Bukoba.
Askofu Msaidizi wa Jimbo la Bukoba, Methodius Kilaini

Kushoto ni Bw. Willy O. Ruta mkurugenzi wa kampuni mpya ya utalii Bukoba Tour akishuhudia Mazishi hayo.

Wengi
 pia walifuatilia kupitia kwenye Tv Screen zilizokuwa ukumbini kutokana 
na wingi wa Watu hivyo Tukio zima kuwafikia kupitia kwenye tv katika 
sehemu walipokuwa maeneo hayo vyema.

Sehemu ya Baadhi ya Wanaumoja













Wageni Mbalimbali kutoka Nje ya Nchi walijumuika

Umati uliojitokeza katika mazishi.

Basi kama tukiishi au kama tukifa, tu mali ya Bwana....Warumi 14:8



























Hakuna maoni:
Chapisha Maoni