Mkurugenzi
 Mtendaji wa Shirika Equality for  Growth (EfG), JaneMagigita 
akizungumza na waandishi wa Habari (Hawapo Pichani) wakati wa ufunguzi 
wa Kongamano hilo Dar es salaam leo.
Ofisa
 Programu Dawati la Uangalizi wa Serikali wa Kituo cha Sheria na Haki za
 Binadamu (LHRC), Hussein Sengu (kulia) akitoa mada katika Kongamano la 
siku mbili la Wanawake Wafanyabiashara Sokoni Tanzania lililofanyika Dar
 es Salaam leo. Kongamano hilo lililowahusisha wanawake kutoka mikoa  tisa ya Tanzania Bara limeandaliwa na Shirika la Equality for Growth (EfG)
Mwezeshaji wa Kongamano hilo, Japhet Makongo akizungumza na Wanawake wafanyabiashara waliohudhuria Kongamano hilo.
Maofisa wa EfG, wakiwa kwenye Kongamano hilo. Kutoka kushoto ni Sarah Mambea na Brenda Kharono.
Maofisa wa EfG, wakiwa kwenye Kongamano hilo, kutoka kulia Mussa Mlawa,Susan Sitta na Munaa Abdalah.
Wafanyabiashara wanawake Masokoni wakiwa kwenye Kongano hilo.
Na Dotto Mwaibale
MKURUGENZI
 Mtendaji wa Taasisi ya Utafiti Tanzania (Repoa), Samwel Wangwe 
amewataka watanzania kuwawezesha wafanyabiashara wadogo wadogo hususani 
wanawake kwani wananafasi kubwa ya kuchangia pato la Taifa.
Akizunguza
 Dar es Salaam leo wakati wa Ufunguzi wa Kongamano la kwanza la wanawake
 wafanyabiashara sokoni Tanzania, Wangwe alisema ni muhimu kuhakikisha 
wafanyabiashara hao wanawezeshwa na kuwajali katika uzalishaji na 
uendeshaji wa biashara zao.
Alisema
 kwa mujibu wa takwimu mbalimbali zinaonesha kuwa hali ya kiuchumi 
duniani katika sekta ya wafanyabiashara wadogo inaendelea kukua hivyo 
kutoa changamoto kubwa katika kuhakikisha inawekewa mazingira mazuri ya 
kisera.
"Wafanyabishara
 wadogo ni wengi sana hivyo wananafasi kubwa ya kuchangia pato la Taifa 
kutokana na uwepo wa asilimia 43 ya wajasiriamali wanawake Tanzania," 
alisema Wangwe.
Kwa
 upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Equality for Growth 
(EfG), Jane Magigita, alisema  lengo la kongamano hilo ni kuwakutanisha 
wanawake wafanyabiashara walio sokoni kutoka katika mikoa mbalimbali ya 
Tanzania Bara kwa lengo la kuwajengea mshikamano na kujadili masuala  muhimu yanayowahusu katika biashara zao.
Alisema
 kongamano hilo limehusisha wanawake 200 kutoka katika mikoa ya Mwanza, 
Shinyanga, Mtwara, Lindi, Mara, Mbeya, Iringa, Dar es Salaam, na mkoani 
Tanga katika Wilaya ya Lushoto huku wakiongozwa na kauli mbiu isemayo 
'Sauti ya Mwanamke Sokoni'.
Alisema
 kauli hiyo inalenga kumkomboa mwanamke mfanyabiashara kwa kumjengea 
uwezo kutambua yeye ni nani na nafasi yake kama raia katika kuendesha 
shughuli biashara za shughuli za soko.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni