Kituo
 Cha Radio Cha Coconut FM Kilichopo Zanzibar Kwa Kushirikiana na Idara 
ya Wanawake na Watoto, Kimeandaa Bonanza linaloitwa "PEPEA - Uhuru Wa 
Nafsi, Akili na Mwili" litakalozinduliwa Jumanne tarehe 16 June, 2015 
SIKU YA MTOTO WA AFRIKA katika Viwanja vya Maisara mjini Unguja kuanzia 
saa 8 Mchana.
Bonanza hili lenye lengo la 
kuhamasisha Wananchi juu ya Kulinda na Kutetea Haki za Watoto Zanzibar, 
linatarajiwa kuhudhuriwa na Wadau Mbalimbali wa Haki za Mtoto, Watoto wa
 Mabaraza ya Watoto, Wazazi, Walezi, Walimu, Wanafunzi, Wanasheria, 
Wanahabari na Viongozi wa Dini, Kuunganisha nguvu pamoja katika Kupinga 
na Kupiga Vita Vitendo vya Udhalilishaji dhidi ya watoto, Ukiukwaji wa 
Haki za Watoto pamoja na "Kutokomeza Ndoa za Utotoni na Mimba za Umri 
Mdogo".
Burudani za Kupambia Tamasha ni IGIZO 
kutoka kwa Watoto wa Mabaraza, Jakaya, Ras Ndaroh, Wakata Minazi Comedy 
pamoja na Ngoma ya Kilua.
PEPEA Bonanza 
litakuwa likifanyika Mara mbili kwa Mwaka, Tarehe 16 June (Siku Ya Mtoto
 Wa Afrika) kila mwaka na Tarehe 20 Novemba (Siku Ya Watoto Duniani) 
Kila mwaka.
PEPEA Bonanza 2015, limefadhiliwa 
na MRADI WA  KILIMO BIASHARA (MIVARF), mradi wenye lengo la 
kuwaunganisha wakulima na masoko na taasisi za fedha, kwa Kushirikiana 
na Coconut Media Group, Kituo Cha Huduma Za Sheria Zanzibar (ZLSC), Cool
 Coco Accessories, Diligent Consulting Ltd, Save The Children, ZIFF 
pamoja na Nyumbani Kwanza Media.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni