HALMASHAURI ZAAGIZWA KUBUNI MIRADI YA MAENDELO

Mahmoud Ahmad Arusha
…………………………………………
Halmashauri za majiji,manispaa,na miji zimeagizwa kubuni vyanzo vya mapato ili kujiongezea uwezo wa kuhudumia miradi ya maendeleo Katika dhana nzima ya kutotegemea misaada ya wahisani.
Kauli hiyo imetolewa wakati wa ufunguzi wa kongamano la upatikanaji wa fedha za ndani za maendeleo lililoandaliwa na mfuko wa umoja wa mataifa wa ukuzaji mitaji(UNCDF)uliofanyika jijini hapa kwa siku mbili.
Akizungumzia umuhimu wa kongamano hilo mratibu wa mashirika ya umoja wa mataifa hapa nchini Alvaro Rodrigeuz alisema kuwa anaipongeza serikali ya Tanzania kwa kufuata mfumo wa ufuatiliaji wa fedha za ndani kwa ajili ya kukuza uwekezaji katika miundombinu ya kibiashara inayoleta mabadiliko kwa umma.
Rodriguez alisema kuwa katika hotuba yake kwamba kwa kuwezesha mfumo wa UNCDF LFI kwenye serikali za mitaa ndio jibu la uhakika la uwekezaji wenye mafanikio endelevu kwa taifa zima huku akitanabaisha kuwa mpango huo wa LFI ambao umekuwepo nchini kwa miaka mitatu sasa umewezesha kuleta mabadiliko katika jamii,na unafaa kumilikiwa na jamii ili kuwezasha mafanikio ya juu katika uwekezaji.
“umoja wa mataifa kupitia UNCDF utaendelea kufanyakazi na serikali ya Tanzania kwa kuamini kwamba vita dhidi ya umaskini itafanikiwa kwa kuhamisha mitaji na kuipeleka katika ngazi za chini kwa maendeleo ya wananchi”alisema Rodrigeuz.
Aidha Kongamano hilo ambalo ni mwendelezo wa uwezeshaji wa kubadilishana uzoefu na elimu kwa lengo la kuwezesha miradi ya umma na binafsi inayochangia maendeleo kujengwa katika siku ya kwanza ya kongamano hili washiriki wataonyeshwa miradi iliyotekelezwa na manispaa ya Busia Uganda na ule wa mji wa Kibaha hapa nchini.
Akisisitiza umuhimu wa kogamano hilo meneja nwa LFI duniani Peter Malika alisema kwamba kongamano hilo linatoa nafasi kwa watumishi wa serikali za mitaa na wengine kujifunza namna mpya ya kupata mitaji kwa kutumia vyanzo vya nyumbani ili kufadhili miradi ya miundombinu ya kiuchumi inayohitajika kwa kutoa fursa za ujasiriamali,biashara,uwekezaji,ajirakuboresha maisha ya watuna ukusanyaji kodi na utoaji wa huduma.
Alisema kuwa washiriki watajadiliana na kujipanga kwa ajili ya utekelezaji wa mfumo huo katika nchi zao wanakotoka il kupiga hatu mbele katika undelezaji wa miradi ya maendeleo inayofadhiliwa na serikali za mitaa bila ya kutegemea fedha za nje.
Aidha Mwakilishi wa Katibu mkuu wa Tamisemi Denis Bandisa alielezea dhamira ya serikali ya kutumia mfumo huo ulioasisiwa na UNCDF kwa kuufanya uwe wa kitaasisi Zaidi ilkuweza kusaidia kuutekeleza mipango ya maendeleo na uwekezaji ya serikali za mitaa.
Bandisa alisifu kazi ya mpango ya uwezeshaji wa fedha za ndani kwa maendeleo(local finance initiative LFI) chini ya sekretarieti ya UNCDF kwa ubunifu wake unaowezesha kupatikana kwa mitaji ya kuwekeza katika miradi ya maendeleo inayofadhiliwa na serikali za mitaa hapa nchini.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni