KAIMU MKURUGENZI WA SHIRIKA LA STAMICO ATEMBELEA MABANDA YA WIZARA YA NISHATI NA MADINI KWENYE MAONESHO YA UTUMISHI WA UMMA JIJINI DAR

Kaimu Mkurugenzi wa Shirika la Madini la Taifa (STAMICO), Mhandisi Edwin Ngonyani (kushoto mwenye suti ya kijivu) akipata maelezo kutoka kwa mtaalam wa Wizara ya Nishati na Madini, Habas Ngulilapi mara baada ya kuwasili kwenye banda hilo katika Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.
Kaimu Mkurugenzi wa Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) Mhandisi Edwin Ngonyani (kushoto) akisaini kitabu cha wageni kwenye banda la Wizara ya Nishati na Madini.
Mtaalam kutoka Kituo cha Jimolojia Tanzania (TGC), Jumanne Shimba ( wa kwanza kulia) akimwonesha Kaimu Mkurugenzi wa Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) Mhandisi Edwin Ngonyani (katikati) moja ya bidhaa zinazotengenezwa na kituo hicho, kwenye banda la Wizara ya Nishati na Madini.
Kaimu Mkurugenzi wa Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) Mhandisi Edwin Ngonyani (katikati) akifurahia moja ya vinyago vinavyotengenezwa na Kituo cha Jimolojia Tanzania (TGC), kwenye banda la Wizara ya Nishati na Madini.
Afisa Uhusiano kutoka Wakala wa Ukaguzi wa Madini Nchini (TMAA), Yisambi Shiwa (kulia) akieleza shughuli zinazofanywa na wakala huo kwa Kaimu Mkurugenzi wa Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) Mhandisi Edwin Ngonyani (Kushoto) mara alipotembelea banda la wakala huo. Katikati ni Omari Rwakyaya kutoka wakala huo.
Kaimu Mkurugenzi wa Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) Mhandisi Edwin Ngonyani (kulia) akisalimiana na Afisa Uhusiano wa shirika la STAMICO, Bibiana Ndumbaro mara alipotembelea banda hilo. Wengine kushoto ni Mhandisi Migodi Mwandamizi, Ibrahim Dauda na kulia ni Mhandisi Uchenjuaji Madini, Pili Athumani.
Mhandisi Migodi Mwandamizi, Ibrahim Dauda (kushoto) kutoka Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) akitoa maelezo juu ya kazi za shirika hilo kwa Kaimu Mkurugenzi wa STAMICO, Mhandisi Edwin Ngonyani (kulia) kwenye banda la shirika hilo.
Kaimu Afisa Masoko Mkuu kutoka makao makuu ya Shirika la Umeme Nchini (TANESCO) (Katikati), Monica Massawe akitoa maelezo kwa Kaimu Mkurugenzi wa Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) Mhandisi Edwin Ngonyani (Kushoto) mara alipotembelea banda la TANESCO. Kulia ni Afisa Uhusiano Wateja –TANESCO Mkoa wa Illala, Lucas Kusare.
Mtaalam kutoka Idara ya Nishati – Wizara ya Nishati na Madini, Jacob Mayala (Kulia) akimweleza Abdul Naseka (Kushoto) majukumu ya Idara ya Nishati kwenye maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.
Kaimu Mkurugenzi wa Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) Mhandisi Edwin Ngonyani (katikati aliyevaa suti) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya washiriki wa maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma kutoka Wizara ya Nishati na Madini.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni