TAARIFA YA OPESHENI USALAMA MBILI MKOANI ARUSHA TAREHE 04/06/2015 NA 05/06/2015



NDUGU WANAHABARI, KWA MUDA WA SIKU MBILI MKOA WA ARUSHA UMEFANYA OPERATION AMBAYO ILIKUWA INAJUMUISHA TAASISI MBALIMBALI ZIKIWEMO POLISI, USALAMA WA TAIFA, TRA , KIKOSI DHIDI YA UJANGILI, IDARA YA MADINI NA UHAMIAJI.
OPERATION HIYO ILILENGA KUKAMATA WAHAMIAJI HARAMU, MAGARI YA WIZI, MADAWA YA KULEVYA, SILAHA HARAMU, USAFIRISHAJI HARAMU WA BINADAMU, WIZI WA MIUNDO MBINU YA TANESCO, UWINDAJI HARAMU WA NYARA ZA SERIKALI, UTOROSHAJI WA MADINI NJE YA NCHI NA MAKOSA MBALIMBALI.
OPERATION HII YA JANA NA LEO IMEONYESHA MAFANIKIO MAKUBWA BAADA YA KUKAKAMATA GUNIA 122 ZA MADAWA YA KULEVYA AINA YA BHANGI, MISOKOTO 700 YA MADAWA HAYO PAMOJA NA KUTEKETEZA HEKARI 15 ZA MADAWA HAYO.
MBALI NA MATUKIO HAYO PIA JUMLA YA KILOGRAMU 28 ZA MADAWA YA KULEVYA AINA YA MIRUNGI ZILIKAMATWA , POMBE HARAMU YA MOSHI LITA 453 ILIPATIKANA PAMOJA NA MAGARI MAWILI  YANAYODHANIWA KUWA NI YA WIZI YALIPATIKANA AMBAYO NI AINA YA TOYOTA HILUX  DOUBLE CABIN NA TOYOTA MARK II.
KATIKA OPERATION HIYO JUMLA YA WATUHUMIWA 14 KUTOKA WILAYA MBALIMBALI ZA MKOA HUU WAMEKAMATWA NA WANAENDELEA KUHOJIWA KWA MAKOSA MBALIMBALI WAKIWEMO WATUHUMIWA WANNE WA KOSA LA KUFANYA BIASHARA BILA LESENI PAMOJA NA MHAMIAJI MMOJA.
AIDHA MTUHUMIWA MMOJA AITWAYE NOEL S/O MESEYEKI MIAKA 20 MKAZI WA MTAA WA SEURI ALIJERUHIWA KWA RISASI KATIKA PAJA LAKE BAADA YA KUPAMBANA NA ASKARI POLISI KWA KUTAKA KUMKATA KWA PANGA WAKATI WAKIENDELEA KUFANYA OPERATION YA MADAWA YA KULEVYA.
MPAKA HIVI SASA NINAVYOZUNGUMZA NANYI OPERATION HIYO BADO INAENDELEA HIVYO NITAZIDI KUWAPA TAARIFA ZAIDI. ASANTENI KWA KUNISIKILIZA.
IMETOLEWA NA KAMANDA WA POLISI MKOA WA ARUSHA,
NAIBU KAMISHNA WA POLISI
(DCP) LIBERATUS SABAS

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni