CHAMA CHA CCM KINAKABILIWA NA KAZI KUBWA YA KUHAKIKISHA KINASHIDA UCHAGUZI WA MWAKA HUU-BALOZI SEIF ALI IDDI.

Mke wa Mbunge wa Kitope Mama Asha Suleiman Iddi akiwanasihi wazazi kuendelea kuwaonyesha njia watoto wao wakati akizungumza kwenye mkutano wa ccm wa Matawi ya Kumbaurembo na Cairo katika Kijiji cha Kiwengwa ndani ya Jimbo la Kitope.Kulia ya Mama Asha ni Mbunge wa Jimbo la Kitope ambae pia ni Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi.
 Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar akimjuilia Hali Muwasisi wa ASP na Muanzilishi wa CCM Bibi Fatma Suleriman Sio Katika Kijiji cha Kiwengwa.
 Balozi Seif ambae pia ni Mbunge wa Jimbo la Kitope akimsalimia Mzee  Haji Muhidini katika Mtaa wa Kumburembo Kiwengwa akiwa katika ziara ya kuwajulia hali Wazee waasisi wa Afro Shirazy Party.
Balozi Seif akisalimiana na Mzee Muasisi wa Afro Shirazy Party Bwana Rashid Khalfan wa mtaa wa  Cairo ndani ya Kijiji cha Kiwengwa Wilaya ya Kaskazini “ B “. Picha na –OMPR – ZNZ.
Mbunge wa Jimbo la Kitope Balozi Seif Ali Iddi alisema kwamba kazi kubwa inayowakabali wana wa Chama cha Mapinduzi katika kipindi hichi kinachoelekea kwenye maandalizi ya Uchaguzi Mkuu wa Mwezi Oktoba mwaka huu ni kuhakikisha kwamba  Chama hicho kinashinda na kuendelea kuongoza Dola.
Alisema sababu za ulazima wa kushinda huko kunatokana na kwamba  amani na utulivu wa Taifa la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania umo ndani ya mikono ya Chama cha Mapinduzi .
Balozi Seif Ali Iddi ambae pia ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM alisema hayo wakati akizungumza na wanachama wa chama cha Mapinduzi wa Matawi ya Kumbaurembo na Cairo yaliyomo ndani ya Kjiji cha Kiwengwa katika Mikutano tofauti.
Alisema Vijana wengi katika baadhi ya maeneo Nchini wamekumbwa na wimbi la Tabia za baadhi ya watu kukashifu wenzao na hata viongozi wa Kitaifa kwa kuwaita majina yasiyostahiki ambayo hata katika maandiko na maamrisho ya Dini hayamo.
Balozi Seif aliwatanabahisha Vijana ambao ndio walio wengi Nchini kuendelea kuwaamini wazazi wao walioshuhudia uchungu na madhila ya Utawala wa Kikoloni pamoja na utamu wa Mapinduzi matukufu ya Zanzibar ya mwaka 1964.
Akigusia suala la ajira Balozi Seif ambar pi ni Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar alisema Nyanja ya ajira bado inaendelea kuwa ngumu si kwa Zanzibar na Tanzania pekee bali hata kwa Dunia nzima kwa ujumla.
Alisema uhimili wa ajira Serikalini bado ni mdogo na ndio maana Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ikaweka mkazo na mipango ya kuimarisha mafunzo ya amali ili vijana wanaomaliza masomo yao ya sekondari wapate fursa za kujiajiri wenyewe.
Mapema Sheha wa Shehia ya Kiwengwa  Bwana Maulid Masoud Ame alisema Shehia hiyo imekumbwa na tatizo kubwa la ukosefu wa huduma za maji kutokana na baadhi ya wawekezaji kushindwa kutekeleza vyema mikataba waliyofunga kati yao na wananchi hao.
Sheha Maulid alisema kumekuwa na ujanja unaoonekana kufanywa na baadhi ya wawekezaji hao baada ya kushindwa kuendesha miradi yao jambo ambalo limetoa mwanya kwa baadhi ya watu kuharibu miundo mbinu iliyopo ya usambazaji wa huduma hiyo baada ya kusita kwa muda mrefu.
Naye Mke wa Mbunge wa Jimbo la Kitope Mama Asha Suleiman Iddi aliwakumbusha wazazi kuendelea kuwaelekeza watoto wao katika kufuata maadili mema yanayokubalika katika jamii na imani za Dini. Mama Asha alisema Watoto wengi hasa katika maeneo tofauti ya uwekezaji wamekuwa wakibadilika tabia siku hadi siku kiasi kwamba hata zile mila na silka zao zinaonekana kuendelea kupotea.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni