Mke
 wa Mbunge wa Kitope Mama Asha Suleiman Iddi akiwanasihi wazazi 
kuendelea kuwaonyesha njia watoto wao wakati akizungumza kwenye mkutano 
wa ccm wa Matawi ya Kumbaurembo na Cairo katika Kijiji cha Kiwengwa 
ndani ya Jimbo la Kitope.Kulia ya Mama Asha ni Mbunge wa Jimbo la Kitope
 ambae pia ni Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi.
 Makamu
 wa Pili wa Rais wa Zanzibar akimjuilia Hali Muwasisi wa ASP na 
Muanzilishi wa CCM Bibi Fatma Suleriman Sio Katika Kijiji cha Kiwengwa.
 Balozi
 Seif ambae pia ni Mbunge wa Jimbo la Kitope akimsalimia Mzee  Haji 
Muhidini katika Mtaa wa Kumburembo Kiwengwa akiwa katika ziara ya 
kuwajulia hali Wazee waasisi wa Afro Shirazy Party.
Balozi
 Seif akisalimiana na Mzee Muasisi wa Afro Shirazy Party Bwana Rashid 
Khalfan wa mtaa wa  Cairo ndani ya Kijiji cha Kiwengwa Wilaya ya 
Kaskazini “ B “. Picha na –OMPR – ZNZ.
Mbunge
 wa Jimbo la Kitope Balozi Seif Ali Iddi alisema kwamba kazi kubwa 
inayowakabali wana wa Chama cha Mapinduzi katika kipindi hichi 
kinachoelekea kwenye maandalizi ya Uchaguzi Mkuu wa Mwezi Oktoba mwaka 
huu ni kuhakikisha kwamba  Chama hicho kinashinda na kuendelea kuongoza 
Dola.
Alisema
 sababu za ulazima wa kushinda huko kunatokana na kwamba  amani na 
utulivu wa Taifa la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania umo ndani ya mikono
 ya Chama cha Mapinduzi .
Balozi
 Seif Ali Iddi ambae pia ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya 
Taifa ya CCM alisema hayo wakati akizungumza na wanachama wa chama cha 
Mapinduzi wa Matawi ya Kumbaurembo na Cairo yaliyomo ndani ya Kjiji cha 
Kiwengwa katika Mikutano tofauti.
Alisema
 Vijana wengi katika baadhi ya maeneo Nchini wamekumbwa na wimbi la 
Tabia za baadhi ya watu kukashifu wenzao na hata viongozi wa Kitaifa kwa
 kuwaita majina yasiyostahiki ambayo hata katika maandiko na maamrisho 
ya Dini hayamo.
Balozi
 Seif aliwatanabahisha Vijana ambao ndio walio wengi Nchini kuendelea 
kuwaamini wazazi wao walioshuhudia uchungu na madhila ya Utawala wa 
Kikoloni pamoja na utamu wa Mapinduzi matukufu ya Zanzibar ya mwaka 
1964.
Akigusia
 suala la ajira Balozi Seif ambar pi ni Makamu wa Pili wa Rais wa 
Zanzibar alisema Nyanja ya ajira bado inaendelea kuwa ngumu si kwa 
Zanzibar na Tanzania pekee bali hata kwa Dunia nzima kwa ujumla.
Alisema
 uhimili wa ajira Serikalini bado ni mdogo na ndio maana Serikali ya 
Mapinduzi ya Zanzibar ikaweka mkazo na mipango ya kuimarisha mafunzo ya 
amali ili vijana wanaomaliza masomo yao ya sekondari wapate fursa za 
kujiajiri wenyewe.
Mapema
 Sheha wa Shehia ya Kiwengwa  Bwana Maulid Masoud Ame alisema Shehia 
hiyo imekumbwa na tatizo kubwa la ukosefu wa huduma za maji kutokana na 
baadhi ya wawekezaji kushindwa kutekeleza vyema mikataba waliyofunga 
kati yao na wananchi hao.
Sheha
 Maulid alisema kumekuwa na ujanja unaoonekana kufanywa na baadhi ya 
wawekezaji hao baada ya kushindwa kuendesha miradi yao jambo ambalo 
limetoa mwanya kwa baadhi ya watu kuharibu miundo mbinu iliyopo ya 
usambazaji wa huduma hiyo baada ya kusita kwa muda mrefu.
Naye
 Mke wa Mbunge wa Jimbo la Kitope Mama Asha Suleiman Iddi aliwakumbusha 
wazazi kuendelea kuwaelekeza watoto wao katika kufuata maadili mema 
yanayokubalika katika jamii na imani za Dini. Mama Asha alisema Watoto 
wengi hasa katika maeneo tofauti ya uwekezaji wamekuwa wakibadilika 
tabia siku hadi siku kiasi kwamba hata zile mila na silka zao 
zinaonekana kuendelea kupotea.




Hakuna maoni:
Chapisha Maoni