Katibu
 Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akilakiwa na Katibu wa CCM mkoa wa
 Kagera Bw. Ali Ame wakati alipowasili katika kata ya Nyakanazi wilayani
 Biharamulo mkoani Kagera wakati akianza rasmi ziara yake ya kikazi ya 
kukagua na kuhimiza utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 
2010 inayotekelezwa na serikali.
 Ziara hiyo itafanyika katika mikoa mitatu ya kanda ya ziwa ambayo ni 
Kagera yenewe, mkoa wa Geita na kisha atamalizia na mkoa wa Mwanza kwa 
kufanya mkutano mkubwa wa kuhitimisha ziara kutembelea nchi zima ikiwani
 mikoa yote ya Tanzania Bara na Zanzibar na majimbo yote ya uchaguzi 
nchi nzima, ambapo amekutana na wananchi na kusikiliza kero mbalimbali 
za wananchi, kuzifuatilia na kuzipatia ufumbuzi ,
Wakizungumza
 katika mkutano wafugaji wa kanda ya Ziwa wamelalamikia wizara ya 
Maliasili na Utalii hasa askari wa wanyamapori ambapo wamesema wamekuwa 
wakikamata mifugo yao na kuwatoza faini kuanzia shilingi laki mbili 
mpaka milioni kumi, Mbaya zaidi wanapodai haki yao wamekuwa wakifanyiwa 
vitendo vya kikatili kupita kiasi jambo ambalo linawakatisha tamaa ya 
maisha kabisa.
Wafugaji
 hao wameongeza kwamba vikao mbalimbali vimeshafanyika zaidi ya 17 
kupitia ngazi zote za kitaifa kasoro kwa Mh. Rais tu ndiyo hatujafika, 
lakini vikao hivyo vyote havijazaa matunda. bado hali ni mbaya na 
manyanyaso yanazidi kuendelea, wamemuomba Katibu Mkuu wa CCM Ndugu 
Abdulrahman Kinana kuwasaidia ili waweze kupata ufumbuzi wa suala hilo 
na wao waweze kuishi na kufanya shughuli zao kwa amani.
Katika ziara zake hizo Kinana amekuwa akiongozana na Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi wa CCM Ndugu Nape Nnauye.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni