| Katibu
 Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi 
Libarata Mulamula akizungumza katika kikao chake cha kwanza na Watumishi
 wote wa Wizara tangu alipoteuliwa na Rais hivi karibuni kuwa Katibu 
Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa. Mkutano huo 
ulifanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere, 
Jijini  Dar es Salaam tarehe 20 Juni, 2015. Pamoja na mambo mengine 
Balozi Mulamula aliwahimiza Watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje kufanya 
kazi kwa bidii, kuwa  na utii, nidhamu pamoja na unyenyekevu ili kufikia
 malengo katika utekelezaji wa majukumu ya Wizara. | 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni