MAWAKILI ARUSHA WAANDAMANA KWENDA MAKAO MAKUU YA POLISI ARUSHA

Mawakili wakiandamana kuelekea makao makuu ya jeshi la polisi na kuahirisha shughuli zao kwenye  mbali mbali mahakamani leo kama walivyokutwa na kamera ya matukio jijini Arusha

MAWAKILI ARUSHA WAANDAMANA BAADA YA MWENZAO KUKAMATWA KWA SHUTUMA ZA UHAINI video & mp3


JESHI la polisi mkoawa Arusha limesitisha maandamano ya wanasheria wa Chama cha wanasheria nchini TLS kanda ya Arusha, ambao walikuwa wakipinga mwenzao kukamatwa na polisi akiwa mahakamani akijiandaa kumtetea mteja wake.


Kaimu kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa Arusha,Yusufu ILembo, amesema mawaklili hao kutoka chama cha wanasheria nchini TLS,kanda ya Arusha walitaka kuandamana kutoka mahakama kuu kanda ya Arusha kwenda kwa kamanda wa jeshi lapolisi mkoa wa Arusha, bila kibali hivyo maandamano hayoyalikuwa ni batili .
Amesema kuwa mnamo Julai 22 mwaka huu wakili wa kituo cha Sheria na haki za binadamu, mkoa wa Arusha,Yusufu Shilinde Ngalula, alikamatwa wilayani Ngorongoro, alikokwenda kutetea mteja wake, mara baadaya kufika Ngorongoro, alikamatwa na tume ya taifa ya jeshi la polisi na vyombo vingine vya usalama.
Alisema kuwa mara baada ya kuhojiwa mtuhumiwa alitakiwa kurudi polisi siku ya pili na  siku ya tatu aliachiwa huru  bila masharti na aliporudia kusambaza ujumbe kupitia mitandao akidai alikamatwa na jeshi la polisi kwa siku tatu mfululizo bila dhamana.
Amesema baada ya kusambaza ujumbe huo jeshi la polisi wilayani Ngorongoro,lilifungua  shitaka dhidi ya wakili huyo, la kutoa taarifa za uongo kwenye mitandao
Ilembo, amesema maandamano yeyote bila kibali ni kosa la jinai na mawakilihao wamefanya kosahilo huku wakitambua kuwa sheria hairuhusu kuafanya maandamano bila kibali na polisi limewaonya  wasirudie tena vinginvyo  watashughulikiwa kwa mjibu wa sheria .
Amesema hakuna aliyeko juu ya sheria hivyo kila mmoja anapaswa kulinda na kuiheshimu sheria  na polisi haitasita kumchukulia mtu yeyote hatua pindi atakapovunja sheria.
Kamanda Ilembo,amesema tume ilipo Ngorongoro kufuatilia tuhuma dhidi ya raia mmoja wa Sweeden SuzanChristina Nordlund, ambae amekuwa akijihusisha kuchonganishajamii za wafugaji wilayani Ngorongoro na kishakupeleka taarifa Ulaya na Amerika kuwa Ngorongoro sio swali na yeyekujipatia mamilioni ya fedha.
Amesema Suzan,amekuwa akijipatia fedha mara baada ya kuanzisha migogoro kati ya makampuni mawili ya uwekezaji ya Thomsoni na OBC, ambapo huchochea migogoro kwa wananchi ili kuwakataa na kisha kuandika taarifa mbaya ambazo zinalenga kuzuia watalii wasitembelee hifadhi ya Ngorongoro kwa madai kuwa sio salama.
Amesema Suzan, amekuwa akifadhili NGOS, 30 zilizopo Ngorongoro ili kiujihusisha na migogoro hiyo  ambayoinaashiriauvunjifu wa amani na kuzuia watalii wasiingie Ngorongoro.

Kamanda, Amesema kuwa Suzan, alishafukuzwa nchini mwaka 2010 KWA p.I,baadaya kubainika kuwa alijihusuisha na migogoro hiyo,na alijea tebna nchini mwaka 2015 ambapo alifukuzwa tena kwa P.I.
Amesema kuwa tayari walimu watatu wa shule za sekondari za serikali wanashikiliwa na polisi kutokana na kujihusisha kwao na uchochezi huo kutokana na kupokea fedha kutokakwa Suzan kwa lengo la kuzidisha migogoro katiya wananchi na wawekezaji.
Amewataja walimu hao kuwa niClintonMshao wa shuleya sekondari Digodigo,Sapuk Maoi, wa shuleya srokndari Loliondo, na mwalimu Samweli Nangirya, wa sekondari ya Ngorongoro.
Amesema tume hiyo imegundua kuwa kuna waandishi wa habari wamekuwa wakilipwa mamilioni ya fedha na mashirika yasiyoya kiserikali wilayani Ngorongoro kwa ajiliya kuandika taarifa za kupotosha kuhusu hali halisi ya mgogoro huo.
Kwa upande wake mwenyekiti wa chama cha wanasheria TLS,kanda ya Arusha, wakili, Akida Modesti ,amekiri kufanya maandamano hayo bila kibali na hiyo inatokana na
shinikizo kutoka kwa mawakili ambao walitaka kumuona kamanda wa polisi mkoa ili kushinikiza mwenzao aachiliwe.Amesema mkurugenzi huyo wa kituo cha haki za binadamu ,kituo cha Arusha Yusufu Ngalula, alikamatwa alipokuwa kwenye mahakama ya wilaya ya Ngorongoro, akijiaandaa kumtetea mteja wake .
Amesema kitendo hicho ni cha uzazililishaji ndio sababu kukawa na shinikizo la kuandamana ,hadi kwa kamanda wa polisi mkoa .
Amesema malalamiko yao mengine ni pamoja na kupungua kwa mahusiano kati ya polisi na mawakili  ambayo yamekuwa ni ya kudharirishana hasawakili anapofika kituo cha polisi kushughulikia maswala ya mteja wake ambae amekamatwa wamekuwa wakidhariruishwa na kutokuthaminiwa.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni