Mbunge
 wa Jimbo la Ilala Mh. Mussa Zungu (wa pili kushoto) akimkabidhi mfano 
wa hundi, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda yenye thamani ya 
Sh. Milioni 27, sambamba na kukabidhiwa madawati 30 kwa Mwenyekiti wa 
Mtaa wa karume, Haji Bechina (kulia) yenye thamani ya milioni 36, hafla 
hiyo ilifanyika Mtaa wa Karume, Jijini Dar es Salaam. wakwanza kushoto 
ni Diwani wa Kata ya Ilala Saady Khimji .
 Mkuu
 wa Mkoa wa Dar es SalaamMh.  Paul Makonda akikata utepe kuashiria 
uzinduzi wa hafla ya kukabidhiwa mfano wa hundi kutoka kwa Mbunge wa 
Jimbo la Ilala, Mussa Zungu yenye dhamani ya Sh. Milioni 27 kwa niaba ya
 uchangianji wa madawati kwa kuitikia wito wa Rais Magufuli na katika 
hafla hiyo mwenyekiti wa Mtaa wa Karume,  Haji Bechina na yeye 
alimkabidhi Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam madawati 30 yenye dhamani ya 
Sh. Milioni 36.
 Mwenyekiti
 wa Mtaa wa Karume,  Haji Bechina akiteta jambo na Mkuu wa Mkoa wa Dar 
es Salaam  Mh. Paul Makonda mara baada ya hafla ya kukabidhiwa hundi ya 
milioni 27 iliyotolewa na Mbunge wa Jimbo la Ilala,  Mh. Mussa Zungu na 
kupokea madawati 30 yenye dhamani ya Milioni 36 kutoka kwa Mwenykiti 
huyo.
 Mkuu
 wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda  akizungumza katika hafla hiyo, 
kulia ni Mwenyekiti wa Mtaa wa karume, Haji Bechina na kuanzia kushoto 
ni Diwani wa Kata ya Ilala Saady  Khimji  na Mbunge wa Jimbo la Ilala 
Mh. Mussa Zungu.
 Mbunge wa Jimbo la Ilala Mussa Zungu akizungumza jambo katika hafla hiyo.
 Mwenyekiti
 wa Mtaa wa Karume,  Haji Bechina (kushoto) akimtambulisha Magreth 
Mwandri (wa pili kushoto) kwa Mh. Paul Makonda ambaye alikuwa Afisa 
Mtendaji wa Mtaa Karume na sasa amehamishiwa Kata ya Kitunda Mtaa wa 
Kitunda Kati
Mh.
 Mkuu wa Mkoa, Paul Makonda akiagana na wananchi mara baada ya 
kukabidhiwa mfano wa hundi yenye dhamani ya Sh. Milioni 27,na Mbunge wa 
Ilala Mussa Zungu na kupokea madawati 30 yenye dhamani ya Milioni 36 
toka kwa Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Karume.
 Mwenyekiti
 wa Mtaa wa karume, Haji Bechina (kulia) akimpokea Mkuu wa Mkoa Paul 
Makonda wakati alipofika katika hafla ya kukabidhiwa mfano wa hundi 
yenye thamani ya Sh. Milioni 27 na Mbunge wa Jimbo la Ilala na kupokea 
madawati 30 yenye dhamani ya Sh. Milioni  36 kutoka kwa Mwenyekiti huyo 
 Wananchi wakiwa katika hafla hiyo
  (PICHA ZOTE NA KHAMISI MUSSA)  
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni