MTU AWAUWA KWA KUTUMIA KISU WAGONJWA WA AKILI 19 NCHINI JAPAN

Wakazi 19 wameuwawa kwa shambulizi la kutumia kisu katika kituo cha kulelea watu wenye ulemavu wa akili katika mji wa Sagamihara nchini Japan.

Mashambulizi ya aina hiyo ni adimu mno kutokea nchini Japan, na tukio hilo limeelezwa kuwa ni baya kuwahi kutokea nchini humo tangu kupita miongo kadhaa.

Polisi wamemkamata mwanaume mmoja ambaye ni mtumishi wa zamani wa kituo hicho, ambaye alijipeleka kituo cha polisi na kukiri kufanya shambulizi hilo.
Kuna taarifa kuwa mtu huyo alinukuliwa akisema alikuwa anataka watu wenye ulemavu kutoweka kabisa.
Polisi wa Japan wakiwa katika eneo la kituo cha walemavu wa akili kilichotokea tukio hilo la kushtusha
Damu zikionekana kwenye uskani wa gari alilotumia muuaji likiwa limeegeshwa nje ya kituo cha polisi baada ya kujisalimisha mwenyewe

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni