KOCHA ANTONIO CONTE ATAMBULISHWA RASMI NA KUAHIDI KUIREJESHEA MAKALI YA CHELSEA

Kocha Antonio Conte ametambulishwa rasmi Stamford Bridge na kuahidi kuifanya kazi yake kwa mapenzi na kuweza kuirejeshea makali yake Chelsea kuweza kutinga katika Ligi ya Mabingwa Ulaya.

Conte ameapa kuwa sasa atachapa kazi katika kuondoa mawazo ya mwenendo mbaya wa msimu uliopita, ambao walijikuta wakiishia katika nafasi ya kumi ya msimamo wa ligi licha ya kuwa mabingwa watetezi.

Akiongea kwa muda wa dakika 45, katika mkutano uliopangwa kati kati ya muda wa mazoezi, Conte amekiri kuwa itakuwa vigumu kupata mafanikio ya mara moja katika mazingira ya ushindani mkali, ila anaimani na mbinu zake. 
                         Kocha Antonio Conte akionyesha jezi ya Chelsea yenye jina lake
Kocha Antonio Conte akiwa amepozi katika picha iliyopingwa akiwa ndani ya uwanja wa Stamford Bridge

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni