MCHUNGAJI WA ZIMBABWE ALIYESHIKILIWA KWA KUITISHA MGOMO WA KITAIFA ATOA WITO MGOMO UENDELEE

Mchungaji nchini Zimbabwe aliyekamatwa kwa muda baada ya kuratibu mgomo wa kitaifa wiki iliyopita ametoa wito kwa watu kuendelea kugoma.

Mchungaji Evan Mawarire ameiambia BBC kuwa watu wanapaswa kuendelea kukaa nyumbani, kama njia ya kampeni dhidi ya rushwa, uchumi mbovu na ukosefu wa ajira.
Mchungaji Mawarire ambaye aliachiwa jana na mahakama baada ya kutupilia mbali mashtaka yake, amesema kampeni hiyo imejidhatiti kuleta mabadiliko nchini humo.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni