SERIKALI ,AZAKI ZASHAURIWA KUZITUMIA TAFITI KUTOKOMEZA NJAA

Image result for azaki 
 
Arusha,Serikali  pamoja na Asasi zisizo za kiraia zimeshauriwa  kuzitumia tafiti mbalimbali za masuala ya kilimo zinazofanywa na  vyuo vya elimu ya juu hapa nchini kama njia ya kusaidia kutokomeza njaa na kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi.

Ushauri huo ulitolewa jana  jijini hapa na baadhi ya wanafunzi wa vyuo vya elimu ya juu kutoka nchini Canada na Tanzania ambao walikuwa wakihudhuria semina ya kimataifa ya mradi wa utafiti wa kilimo utakaochukua  wiki tano kuanzia Julai 14 hadi Agosti 19 mwaka huu.

Jumla ya wanafunzi 16 kutoka Tanzania na Canada wamekutana katika semina  hiyo inayofadhiliwa na taasisi ya World Univesity Service of Canada(WUSC) kama fursa njia ya kutoa fursa kwa  wataalamu wachanga kutoka nchi hizo mbili kubadilishana uzoefu katika maswala mbalimbali ya maendeleo.

Wakizungumza kwa nyakati mara baada ya kufunguliwa kwa semina hiyo na mkuu wa wilaya ya Arusha,Mrisho Gambo baadhi ya wanafunzi walioshiriki semina hiyo walisema kwamba tafiti nyingi duniani zimesaidia kuleta mageuzi ya kilimo na kutatua  changamoto ya mabadiliko ya tabia nchi.

Kathleen  Novelia,ambaye ni mwanafunzi wa chuo kikuu cha Ryerson nchini Canada aliwaambia waandishi wa habari kwamba  tafiti nyingi zimesaidia mataifa mbalimbali duniani zilizotiliwa mkazo zimesaidia kutatua  kero mbalimbali hususani katika masuala ya usalama wa chakula.

“Ni jambo zuri kubadilishana uzoefu  imani yangu ni kwamba kupitia semina hii tutaibuka na njia za kukabiliana na tatizo la usalama wa chakula naamini tutakuja na mapendekezo na ushauri”alisema Novelia

Hatahivyo,Samwel Lucas ambaye ni mhitimu wa chuo kikuu cha Kikatoliki cha Mwenge kilichopo  mkoani Kilimanjaro hapa nchini alisema kuwa serikali pamoja na Asasi zisizo za kiraia zinaweza kunuifaika na tafiti nyingi zinazofanya na  vyuo mbalimbali nchini kama njia ya kubuni njia rafiki katika sekta ya kilimo .

“Kuna faida nyingi kwa serikali pamoja na Azaki kwa kuwa tafiti hizi zinasaidia sana kubuni njia rafiki katika sekta ya kilimo,mbogamboga na matunda”alisisitiza Lucas

Awali mratibu wa semina hiyo kutoka taasisi ya Wusc,Christina Sudi alisema kwamba wanafunzi hao watakuwa pamoja na muda wa wiki tano kuanzia juzi kufanya utafiti katika mabadiliko ya tabia nchi,teknolojia na usalama wa chakula katika mikoa ya Arusha,Kilimanjaro na Manyara.

Alisema kwamba utafiti huo utasaidia kuleta mabadiliko chanya katika jamii mbalimbali hapa  nchini ambapo ripoti ya utafiti wao ikishakamilika itawasilishwa serikalini kwa lengo la kuisaidia kuleta mageuzi ya kilimo hapa nchini Tanzania na Canada.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni