MAKUMI WAZIMIKA MITAANI BAADA YA KUJIZIDISHIA DOZI YA BANGI MAREKANI

Ilikuwa kama kwenye filamu ya wafu wanaotembea, na pengine mazombi wasioweza kutembea pale makumi ya watu walipozidisha kiwango cha bangi na kuishiwa nguvu na kubakia kama mazezeta huko Brooklyn, Marekani.

Watu wapatao 33 walilazwa kutokana na uwezekano wa kujizidishia dozi ya kileo aina ya K2, ambacho ni aina ya bangi, katika eneo la Brooklyn, Marekani.

Mashahidi wamesema waliona makumi ya watu wakiwa wamepoteza fahamu, wakitapika, kujisaidia haja ndogo kati kati ya barabara majira ya saa tatu na nusu asubuhi kwenye mitaa ya Bedford-Stuyvesant.
Mmoja wa watu waliotumia bangi hiyo akiwa amezimika juu ya boneti la gari lililoegesha
  Huyu naye alikutwa akiwa amezimika kati kati ya magari yaliyokuwa yameegesha

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni