MKUU
 WAPOLISI  WILAYA YA ARUSHA( SSP)EMMANUEL TILLE AKIZUNGUMZA NA VIONGOZI 
WA KATA YA MOIVARO TARAFA YA SUYE NA PAMOJA NA ASKARI WA ULINZI 
SHIRIKISHI WAKATI WA UZINDUZI WA VIKUNDI VINNE VYA KATA HIYO.
 Jeshi
 la Polisi linaendeleza harakati za kupambana na uhalifu ili kupunguza 
matukio ya namna hiyo, wananchi wa kata ya Moivaro tarafa ya Suye 
halmashauri ya jiji la Arusha hawapo mbali na jitihada hizo hivyo kuamua
 kujitokeza kwa moyo mmoja kupinga uhalifu kwa kuanzisha vikundi vinne 
vya ulinzi shirikishi kutoka mitaa ya Ngurumausi, Oldonyommasi, Moivaro 
Kati na Shangarao.
Akizindua
 vikundi hivyo ambavyo vimewezeshwa na wadau walioongozwa na Jeff Mligha
 ambao walijitolea vifaa mbalimbali vya ulinzi zikiwemo tochi, Mkuu wa 
Polisi wilaya ya Arusha Mratibu Mwandamizi wa Polisi Emmanuel Tille kwa 
niaba ya Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha alisema kwamba matarajio ya 
wananchi katika kata hiyo ya Moivaro ni makubwa na ana imani watakuwa 
wanalala na kuamka salama hivyo kuwataka walinzi hao wawe na nidhamu 
kwenye kazi yao.
“Kazi
 ya ulinzi ina miiko yake; kitu cha kwanza ni nidhamu ya hali ya juu. 
Mimi mwenyewe mpaka nafikia hatua hii ni kwa sababu ya nidhamu na 
nawataka ninyi muige mfano wangu, ninachosema hapa ni pamoja na kuwahi 
kazini, kutunza siri pasipo kuwazunguka wenzako pamoja na kufuata 
maelekezo ya wakubwa wa vikundi vyenu” Alisisitiza Tille.
Amesema
 japokuwa askari hao wapatao 42 wamepewa mafunzo lakini kupitia Wakaguzi
 wa Polisi wa Tarafa na askari kata wataendelea kuwapa mafunzo mara kwa 
mara ili waweze kufanya kazi zao kwa mujibu wa sheria, huku akiwaonya 
wasijichukulie sheria mkononi.
Amewataka
 wananchi wanapopata taarifa watoe kwa viongozi wa Polisi mara moja ili 
ziweze kufanyiwa kazi kwa haraka na hatimaye kufikia malengo ya 
kupunguza uhalifu ndani ya jiji la Arusha, huku akiwataka watendaji wa 
kata na Wakaguzi wa tarafa wahakikishe askari wa kata wanakuwa katika 
maeneo yao kila siku hali ambayo itawasaidia kubaini maeneo tete.
Akizungumza
 katika uzinduzi huo Diwani wa kata hiyo Rick Moiro alivitaka vikundi 
hivyo kufuata taratibu za kazi na kupambana na uhalifu hasa vijana 
wanaojihusisha na madawa ya kulevya aina ya bangi huku akiomba Jeshi la 
Polisi litoe ushirikiano wa karibu na vikundi hivyo pindi tu wanapoomba 
msaada.
 Afisa
 Mtendaji wa kata hiyo Bi. Editha Kisangia alisema kwamba mbali na hali 
ya uhalifu kuwa ya kawaida katika eneo hilo lakini hatarajii kutokea kwa
 changamoto kutoka kwa baadhi ya wananchi kushindwa kuchangia vikundi 
hivyo kwani faida wataiona baada ya kuanza kufanya kazi.
Wakaguzi
 wa Polisi wanaoongoza tarafa tatu za halmashauri ya jiji la Arusha toka
 mwaka 2013 ni pamoja na Frimina Massao tarafa ya Suye, Winibrita Moshi 
tarafa Elerai na Shabani Shabani tarafa ya Themi.
MKUU
 WA POLISI WILAYA YA ARUSHA( SSP) EMMANUEL TILLE AKIWAKAGUA ASKARI WA 
VIKUNDI VYA  ULINZI SHIRIKISHI KUTOKA MITAA YA 
NGURUMAUSI,OLDONYOMMASI,MOIVARO KATI NA SHANGARAO.
DIWANI
 WA KATA YA MOIVARO RICK MOIRO AKIZUNGUMZA NA VIKUNDI VYA ASKARI WA 
ULINZI SHIRIKISHI WALIOTOKA KWENYE BAADHI YA MITAA YA KATA YAKE BAADA YA
 UZINDUZI WA VIKUNDI HIVYO.
MMOJA
 WA WAHITIMU WA MAFUNZO WA VIKUNDI VYAASKARI WABULINZI SHIRIKISHI 
 AKIKABIDHIWA KITAMBULISHO CHA KAZI NA MKUU WA POLISI WILAYA 
(SSP)EMMANUEL TILLE.
BAADHI
 YA VIONGOZI WA KATA YA MOIVARO PAMOJA NA VIKUNDI VIPYA VYA  ASKARI WA 
ULINZI SHIRIKISHI WAKIMSIKILIZA MKUU WA POLISI WILAYA YA ARUSHA 
(SSP)EMMANUEL TILLE.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni