WAZIRI WA UCHUKUZI ATEMBELEA VIWANJA VYA NDEGE JIJINI DAR ES SALAAM

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa (kushoto), akizungumza na wafanyakazi wa Kampuni ya kuhudumia mizigo, Ndege na abiria ya Swissport inayotoa huduma katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA), alipofanya ziara ya siku moja ya kutembelea uwanja huo Dar es Salaam leo.
Kamanda wa Polisi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA), Kamishna Msaidizi (SACP), Martin Otieno (kulia), akimueleza Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa (kushoto), kuhusu hali ya usalama katika uwanja huo wakati wa ziara ya waziri huyo katika uwanja huo Dar es Salaam leo. (Katikati) ni Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Mhandisi George Sambali,
Ofisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Swissport, Gaudence Temu (wa pili kushoto), akimuelekeza Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa (wa pili kulia), jinsi kampuni hiyo inavyofanyakazi na changamoto zake. Kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Mhandisi George Sambali. Kushoto ni Meneja Biashara wa TAA, Efata Lyimo.
                                                           Vifufushi vikiwa kwenye ghara jipya la Swissport.
                                   Foku lifti likifanya kazi ya kubeba mizigo katika ghara hilo.
Kamishna Msaidizi wa Uhamiaji, Elizabeth Lukuwi (kushoto), akutoa maelezo kwa Waziri Mbarawa baada ya kufika eneo la ukaguzi kwa wageni.
Kamishna Msaidizi wa Uhamiaji, Elizabeth Lukuwi, akimpigia saluti Waziri Mbarawa baada ya kumpa maelekezo ya utendaji kazi katika kitengo cha wageni kiwanjani hapo.
Waziri Mbarawa akizungumza na Raia wa Kigeni aliyemuelezea kutumia muda mwingi zaidi ya masaa mawili kwa ajili ya upimaji wa afya uwanjani hapo ambapo Waziri huyo aliwaagiza wahusika kuhakikisha wanatumia muda mfupi kutoa huduma kwa wageni ambao wanakuwa wamerundikana katika eneo hilo.
                                             Baadhi ya wafanyakazi wa JNIA wakiwa uwanjani hapo.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni