WAZIRI MKUU DAVID CAMERON AAGWA BUNGENI KWA HESHIMA KUBWA

Wabunge wa chama cha Conservative wamesimama wima wote bungeni ikiwa ni heshima kwa Waziri Mkuu wa Uingereza David Cameron baada ya kumaliza kipindi chake cha mwisho cha maswali na majibu kabla ya kuachia madaraka.

Waziri Mkuu Cameron, baadaye leo ataenda kwenye makazi ya malkia huko Buckingham Palace, kuwasilisha rasmi barua yake ya kujiuzulu wadhifa wake kwa Malkia Elizaberth wa pili.

Akitetea mafanikio yake akiwa madarakani Cameron amesema kilikuwa ni kipindi mambo yenyekuvutia wakati wote wa miaka sita iliyopita akishikilia wadhifa huo.
Waziri wa Mambo ya Ndani Theresa May, anajianda kuchukua madaraka kutoka kwa Cameron baadaye baada ya kukutana na Malkia.
Wabunge wa Conservative wakiwa wamesimama juu na kupiga makofi wakimuaga Waziri Mkuu David Cameron

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni