MILIPUKO MIKUBWA YATOKEA KARIBU NA UWANJA WA NDEGE WA MOGADISHU

Milipuko mikubwa iliyofuatiwa na milio ya risasi imesikika karibu na lango kuu la kuingilia uwanja wa ndege wa Jiji la Mogadishu nchini Somalia.

Moshi mzito umeonekana ukipanda juu kutoka katika eneo hilo, ambalo pia lina kambi ya walinda amani wa Umoja wa Afrika.

Waandishi wa nchini Somalia wamesema milipuko hiyo imesababishwa na mabomo mawili.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni