MTOTO ALIYESAIDIWA NA RAIS KENYATTA KWENDA INDIA KWA MATIBABU AZUIWA HOSPITALINI

Mtoto wa kiume aliyewezeshwa na rais Uhuru Kenyatta kusafiri India kwa matibabu ya kupandikizwa figo amekwama nchini humo baada ya familia yake kushindwa kupata shilingi milioni 2.8 za Kenya ili kulipia bila ya hospitali.

Hospitali ya Artemis iliyopo Haryana inashikilia hati za kusafiria za mama na mtoto huyo Brian Karuga na Bi. Ruth Njeri, pamoja na nyaraka nyingine mbalimbali za kusafiria tangu Juni 20, mwaka huu.

Bi. Njeri amesema walilazimishwa kukabidhi nyaraka hizo kutokana na kutokuwa na kiasi chote cha shilingi milioni 6 za Kenya zilizokuwa zinahitajika na hospitali hiyo ya India kwa ajili ya gharama za matibabu.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni