NYOTA WA KIKAPU MAREKANI WATAKA MAUAJI YA KUTUMIA BUNDUKI YAKOME

Nyota wa Mpira wa Kikapu Marekani (NBA) wameomba kumalizika kwa matukio ya mauaji ya kutumia bunduki pamoja na mauaji yanayofanywa na polisi yenye mrego wa kibaguzi kwa weusi nchini humo.

Wito huo umetolewa na nyota wa kikapu LeBron James, Carmelo Anthony, Chris Paul na Dwyane Wade katika hutuba yao wakati wa hafla ya utoaji Tuzo kwa Wanamichezo Bora wa mwaka (ESPY) Jijini Los Angels.

Wakiongea kwa nyakati tofauti kufuatia matukio ya hivi karibuni ya kuuwawa na polisi Wamarekani weusi wawili, nyota hao wa kikapu wamesema imetosha sasa na ni wakati wa kukomesha mauaji ya aina hiyo.
                                     LeBron James akiongea kwa hisia kali katika hafla hiyo

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni