Shule ya kwanza kitaifa yahitaji msaada

Image result for kisimiri high school
SHULE ya Sekondari Kisimiri iliyoshika nafasi ya kwanza  Kitaifa kwa matokeo ya kidato cha sita iliyopo wilayani Arumeru ,Mkoani Arusha inahitaji  shilingi milioni 900, kwa ajili ya ujenzi wa uzio na mabweni ili kuwanusuru wanafunzi wanao ishi shuleni hapo wasiliwe na wanyama wakali wanao randa randa nyakati za usiku .

Hayo yalibainishwa mwishoni mwa wiki na mkuu wa shule hiyo mwl,Emmanuel Kisongo alipo tembelewa na ,Mkurugenzi wa Halmashauri ya Meru , Japhet Kazeri kwa lengo la kumpongeza na kumkabidhi cheti maalumu baada ya kuitoa kimaso maso Halmashauri yake.
Kisongo alisema kuwa shule hiyo pamoja na kufanya vizuri kwenye matokeo ya mitihani, haijawai kupewa msaada wowote na serikali ila jitihada za waalimu zimesaidia kuifikisha shule hiyo ilipo na kufanya vizuri kwa miaka 8 na kwa mwaka huu imevunja  rekodi kwa kushika nafasi ya kwanza Kitaifa

“Ni vizuri serikali ikaangalia uwezekano wa kutusaidia hili kuondoa changamoto zinazo tukabili tunahitaji kiasi cha shilingi milioni 900, kujenga uzio kujenga mabweni na kukarabati miundo mbinu yetu ‘’Alisema Kisongo. 

Katika hatua nyingine Kisongo alisema kuwa tangu shule hiyo ishike namba moja Kitaifa amekuwa akikabiliwa na changamoto nyingi kwa wazazi kuomba nafasi kuhamishia watoto wao katika shule hiyo , pia alidai baadhi ya wamiliki wa shule binafsi wamekuwa wakimpigia simu kumrubuni ahamie kwenye shule zao.

Aidha Kisongo alimshukuru   Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo kufika katika shule hiyo  kumpongeza na kujionea changamoto zilizopo na kueleza siri ya mafanikio ya shule hiyo pamoja na walimu kujituma pamoja na usimamizi wake na kufuatilia mienendo za walimu juu ya ufundishaji madarasani .

Kwa upande wake mkurugenzi wa Halmashauri ya Meru Japhet Kazeri, pamoja na kuipongeza shule hiyo kwa kuitoa kimaso maso halmashauri hiyo alikabidhi cheti  maalum kwa mkuu wa shule hiyo na kuahidi  kutatua changamoto ya bara bara  yenye urefu wa kilometa 7 inayo elekea shuleni hapo  kwa kutengeneza katika  kiwango cha changarawe .

Hata hivyo alisema ni jukumu la serikali kutunza mazingira na miundo mbinu za shule zinazo fanya vizuri hasa katika matokeo ya mitihani.

Kwa upande wake Afisa elimu wa shule za sekondari wa halmashauri hiyo mwl. Damari Mchome alisema tangu shule hiyo kuibuka kinara wa ufaulu kitaifa ofisi yake imepokea maombi ya barua zaidi ya 700 kwa wazazi kuomba watoto wao kuhamia katika shule hiyo.
Mchome alisema kuwa shule hiyo yenye wanafunzi 1117 na walimu 68 kwa sasa haina nafasi ya kuchukua wanafunzi wapya huku akiwataka wazazi wawe na subira.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni