Makamu
 wa Rais wa Huduma wa Shirika la Ndege la Etihad, Sajida Ismail, Makamu 
wa Rais wa Uhusiano wa shirika hilo, Calum Laming akipokea tuzo za 
Skytrax World Airline ya World Best First Class Airline, World’s Best 
First Class Onboard Catering na World’s Best First Class Airline Seat
Shirika
 la ndege la Etihad limetunukiwa tuzo tatu za ubora wa juu kwenye 
madaraja  pia tuzo ya ubora kwenye huduma za vyakula pia  tuzo ya ubora 
kwenye malazi  kutoka Skytrax Worldairline Awards, zilizotangazwa NCHINI
 uingereza.
Tuzo 
hizo za World Airline ni za kimataifa na huhusisha mashirika ya ndege 
yanayofanya vizuri katika sekta ya usafiri wa anga. Mshindi huchaguliwa 
kwa kura kutokana na mchakato ambao huchukua miezi 10 kukamilika kwake 
huku ikujumuisha wasafiri takribani milioni 18 kutoka katika nchi zaidi 
ya 100 ulimwenguni.
Makamu
 wa Rais wa Shirika la Etihad kwenye masuala ya wageni alisema,“ Mwaka 
2014 tuliingia kwenye ushindani kwa kutambulisha ndege yetu ya abiria 
Airbus A380 na Boing 787 Dreamliner. Jambo hili limeonyesha dhamira yetu
 ya kuwa wa kwanza katika kutoa huduma ya kisasa na uvumbuzi.”
“Ninafarijika
 na jambo hili ikiwa ni matokeao ya uwekezaji wa huduma bora kwa wateja 
wetu ulimwenguni, kwa mara nyingine tena tumetunukiwa tuzo hizo za kuwa 
wa kwanza kwa ubora katika huduma za kuwa na madaraja yenye hadhi.  Tuzo
 hii itakuwa chachu katika kuongeza nguvu kwenye kuwekeza zaidi kwenye 
bidhaa zetu na huduma za usafiri.”
Katika
 miaka ya hivi karibuni, shirika laetu limepata tuzo ya kuwa wa kwanza 
kwenye huduma zetu. Hii ni mara ya pili kwa kupata tuzo na kipekee 
kupata tuzo tatu kwa pamoja ikiwa ni shirika pekee kunyakua tuzo hizo.
Mwnyekiti
 wa Skytrax, Edward Plaisted alisema “Shirika la Ndege la Etihad 
limekuwa likiimarika na kuwa bora zaidi katika usafiri wa anga kwa 
kuendana na mabadiliko ya teknolojia ya kisasa katika utoaji wa huduma 
zake na ukarimu. Kwa mara nyingine tena shirika hili limenyakua tuzo 
tatu muhimu kwa kupigiwa kura na amamilioni ya wasafiri ulimwenguni 
kote, ambapo ni dhahili ilistahili kuwa mshindi kutokana na kutoa huduma
 za kiwango cha juu.”
Kuwapo
 kwa huduma nzuri za maradhi kwa wasafiri, vyumba nanae vya kulala vya 
hadhi ya juu, eneo zuri na la kipekee kwa abria kupumzika likiwa na 
ukubwa wa kutosha ni mambo yaliyopelekea kupata tuzo ya ubora.
Kuwapo
 kwa ndege ya 787 ambayo ina ambayo imesheheni vitu mbalimbali ndani 
yake ikiwamo vyumba vyenye vitanda, runinga kubwa ya kisasa, eneo la 
kulia chakula na madhari ya kuvutia ni miongoni mwa mambo yaliyoipa tuzo
 ya kuwa wa kwanza kwenye ubora wa hali ya juu.
Shirika
 la Ndege la Etihad kwa kutumia ndege zake za Boeing 777 ana Airbus 
A330/A340 itaendelea kutoa huduma bora kwa wateja zikiwa na viti vyenye 
mwonekano na mazingira mzuri kwa mtumiaji.
Ndege 
za shirika la Etihad zimekuwa zikitoa huduma bora zaidi za hoteli ndani 
ya ndege zake ili kukidhi mahitaji ya wateja wake. Katika hoteli zake 
ndani ya ndege kuna huduma ya vyakula vya aina mbalimbali ambavyo 
vinaandaliwa na watu wenye uzoefu. Na huduma ya chakula inatolewa kwa 
madaraja yote kwenye ndege za Etihad. Pia wateja wana fursa ya 
kujadiliana na watoa huduma kwenye ndege kulingana na mahitaji yao ya 
chakula.
Wageni wanaweza kuchagua chakula wanachokipenda kwenye menu zinazopatikana kwenye hoteli za kwenye ndege.
Aidha 
katika Uwanja wa Kimataifa wa Abu Dhabi kumefunguliwa mgahawa ambao 
utahudumia wateja wa Etihad ukiwa na vitu mbalimbali muhimu ambavyo 
vitakidhi mahitaji ya mteja ikiwa na lengo kila mteja apate huduma bora 
inayomfaa.

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni