NMC ARUSHA NI MALI YA SERIKALI

Image result for national milling corporation tanzania
Na Mahmoud Ahmad Arusha
SERIKALI,imesema kuwa kinu cha kusaga mazao cha shirika la taifa la usagishaji,NMC ,cha Arusha hakijauzwa kama ilivyoenezwa na kitaendelea kuwa mali ya serikali na kwamba anaendesha kinu hicho ni mpangishaji na si vingine.
 
Hayo yameelezwa na msajili wa Hazina, Lawrance Mafuru, alipokuwa akikabidhi umiliki wa kinu hicho  cha  kusaga nafaka cha NMC ,cha Arusha kutoka kwa shirika hodhi la mali za serikali, CHC,kwenda kwa bodi ya Nafaka na mazao mchanganyiko. .
 
Mafuru, amesema uamuzi huo wa kukabidhi umiliki wa kinu hicho kwa bodi ya nafaka na mazao mchanganyiko ni maelekezo ya serikali kwa ajili ya kukiendeleza kinu hicho na vingine vilivyopo, Mwanza, Iringa na Dodoma.
 
Amesema kuwa bodi hiyo ambayo ni mmiliki mpya itakuwa na jukumu la kukiendesha kinu hicho  itapitia mkataba wa upangaji na kampuni ya uwekezaji ya Monaban Trading Company limited kwa kuwa hiyo ni sehemu ya biashara.
 
 Amesema kabla ya kukikabidhi kinu hicho kwa mmiliki mpya  walijiridhishwa kwa kufanya  uhakiki wa vitu vilivyopo.
 .
Mafuru,amevitaja vinu vingine ambavyo havitabinafisishwa na vitabakia kuwa ni mali ya serikali ni pamoja na shirika la usagishaji la taifa NMC, Mwanza, NMC,Dodoma na NMC,Iringa ,ambavyo navyo vimekabidhiwa kwa mimiliki mpya ambayo ni bodi ya nafaka na mazao mchanganyiko.
 
Ameongeza kuwa kinu hicho cha NMC ,Arusha, kilipangishwa mwaka  2008 kwa kampuni ya Monaban Trading limited,kutokana na uamuzi wa serikali uliofanywa kwa wakati huo lakini sasa  mali zote za shirika la usagishaji la taifa hazitauzwa zitabakia kuwa mali ya serikali.
 
Nae Kaimu mkurugenzi mkuu wa bodi ya nafaka na mazao mchanganyiko, John Damasi  Maige, amesema bodi hiyo itasimamia shughuli zote za kinu hicho pia watazingatia mkataba unaomwezesha mpangaji kampuni ya Monaban  kuendesha kinu hicho.
 
Amesema kuwa  mara baada ya kupitia mkataba na mpangaji ambae ni kampuni ya Monaban Trading Compan Limited,kuna mambo watakubaliana kwa masilahi ya pande zote mbili.
 
Maige, amesema kuwa bodi ya nafaka na mazao mchanganyiko  inaendesha maghala yaliyopo Dodoma, na kufufua mashine za kusagisha zilizopo NHC Mwanza,ambacho kilikuwa ni kwa ajili ya kusagisha  na kusindika mpunga, kinu cha Dodoma kilikuwa cha kusagisha na kusindika mtama .
 
Lengo la kuvifufua  ni kuviwezesha kufanya kazi na hivyo kutoa ajira hasa kwa vijana ambao ni nguvu kazi ya taifa .
 
Kwa upande wake mwenyekiti wa bodi ya kampuni ya Monabani Trading Limited, Gerad Mandala, amesema watashirikiana na mmiliki mpya kwa kuwa kinu hicho ni mali ya serikali na kiwanda kitaendelea  kama kawaida.
 
Akawaondoa hofu wananchi kwa kueleza kuwa kampuni ya Monaban ni mpangaji na ina mkataba wa muda mrefu  na itaendelea kuwa msagishaji wa nafaka na mazao mengine hivyo wananchi wataendelea kupata huduma ya unga na mahitaji mengine kama kawaida..
 
MWISHO

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni