Na Adili Mhina
Waziri
 wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalim 
amesema kuwa serikali iko mbioni kupeleka bungeni muswada wa marekebisho
 ya sheria ya ndoa ya mwaka 1971 ili kutotoa mwanya kwa watoto wa kike 
kuolewa katika umri wa chini ya miaka 18.
Mhe.
 Ummy ameyasema hayo katika sherehe za kuadhimisha siku ya idadi ya watu
 duniani ambaazo huadhimishwa tarehe 11 Julai kila mwaka.
Waziri
 wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalim 
(Mb) akitoa hotuba yake katika sherehe za kuadhimisha siku ya idadi ya 
watu zilizofanyika Julai 11 katika viwanja vya Mnazi Mmoja, jijini Dar 
es Salaam.
Kwa 
hapa nchini, sherehe hizo zimefanyika katika viwanja vya Mnazi Mmoja 
jijini Dar es Salaam ambapo mgeni rasmi alikuwa Waziri wa Afya, 
Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto na kuhudhuriwa na 
wawakilishi mbalimbali kutoka serikalini, mashirika ya umoja wa mataifa 
pamoja na mashirika yasiyokuwa ya kiserikali.
Katika
 hotuba yake kwenye sherehe hizo zilizotawaliwa na kauli mbiu ‘wezesha 
msichana afikie ndoto zake’, Waziri Mwalim alisema serikali imejipanga 
vizuri kuhakikisha haki za watoto wa kike zinalindwa hivyo ni lazima 
kila mwanachi aelewe umuhimu wa kumlinda mtoto wa kike na kuachana na 
mila potofu.
Mkurugenzi
 Mkuu Ofisi ya Taifa ya Takwimu, Dkt. Albina Chuwa akitoa neno la 
shukrani kwa mgeni rasmi katika maadhimisho ya siku ya idadi ya watu 
duniani.
“Hata
 hivyo pamoja na sheria hizi nzuri tatizo la mimba za utotoni 
halitokwisha kama jamii haitabadilika kuhusu mtizamo hasi walio nao 
baadhi ya watu kuhusu wasichana. Watoto wakike wanatakiwa kuwa shuleni 
na kupata taarifa sahihi za msingi kuhusu afya zao na kuondoa 
unyanyapaa, “ alisema Waziri Ummy.
Waziri
 Ummy alieleza kuwa kulingana na sensa ya watu na makazi ya mwaka 2012, 
Tanzania inakadiriwa kuwa na wasichana wadogo milioni 3.4 (wenye umri 
kati ya miaka 13 hadi 19) sawa na asilimia 7.6 ya watanzania wote na 
hivyo idadi hii haiwezi kupuuzwa katika mipango mbalimbali ya Taifa.
Waziri
 wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto mhe. Ummy Mwalim 
akipata maelezo kutoka kwa moja ya washiriki wa maadhimisho ya siku ya 
idadi ya watu duniani.
Waziri
 Ummy pia alitoa pongezi kwa Tume ya Mipango hususani kwa Kaim katibu 
Mtendaji Bibi Florence Mwanri kwa jitihada zake za kuhakikisha masuala 
ya watoto yanaendelea kutambuliwa zaidi na yanafungamanishwa na 
maendeleo ya uchumi wa nchi.
“Katika
 kipindi cha miaka sita niliyokaa bungeni nilikuwa sijawahi kuona waziri
 wa Fedha anawekea msisitizo masuala ya kukabiliana na ndoa za utotoni 
na kuyafungamanisha na maendeleo ya uchumi. Naamini hizi ni jitihada 
ulizofanya kuhakikisha masuala haya yanatambulika kwa upana zaidi, 
hongera sana Kaim Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango kwa kazi yako 
nzuri”,. Alisema Waziri Ummy.
Kaim
 Katibu Mtendaji Tume ya Mipango, Bibi Florence Mwanri amesema kuwa 
katika kutekeleza mpango wa maendeleo wa miaka mitano wa sasa 
(2016/17-2020/21) unaohimiza uchumi wa viwanda ni lazima kuwekeza vizuri
 kwa watoto wa kike kwa kuwa ndio nguvu kazi ya kesho inayotarajiwa 
kuendesha uchumi wa viwanda.
Bibi
 Mwanri alisisitiza kuwa watoto wa kike wakilindwa na kupatiwa elim 
bora, taifa litakuwa na faida kubwa kwani hapo baadae wataweza 
kujitegemea na kuendesha maisha yao wenyewe, vile vile wataweza kusaidia
 jamaa na familia zao na pia watakuwa na mchango mkubwa katika pato la 
taifa.
Kwa 
sasa wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa 
kushirikiana na Tume ya Mipango pamoja na Ofisi ya Taifa ya Takwimu 
wanaandaa utaratibu wa kutoa elim nchi nzima juu ya masuala ya watoto wa
 kike hususan mimba za utotoni ili kuondokana na tatizo hilo.
Waziri
 wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalim 
(Mb) akisaini daftari la wageni katika banda la Ofisi ya Taifa ya 
Takwimu wakati wa sherehe za maadhimisho ya siku ya Idadi ya Watu 
Duniani ambapo , sherehe hizo zilifanyika katika viwanja vya Mnazi Mmoja
 jijini Dar es Salaam.
Waziri Ummy Mwalim akiangalia picha na maelezo mbalimbali katika banda la Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania (TAMWA).
Mhe.
 Ummy Mwalim akisoma jarida katika moja ya mabanda ya wadau 
waliohudhuria sherehe za siku ya idadi ya watu duniani katika viwanja 
vya Mnazi Mmoja, jijini Dar e s Salaam.
Kaimu
 Katibu Mtendaji Tume ya Mipango, Bibi Florence Mwanri akimwonesha jambo
 Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango Zanzibar bw. Juma Reli wakati wa 
sherehe zakuadhimisha siku ya idadi ya watu duniani.
Waziri
 wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalim 
(watatu kutoka kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na viongozi 
waandamizi wa serikali, wawakilishi wa mashirika ya kimataifa pamoja 
wawakilishi wa mashirika yasiyokuwa ya kiserikali wakati wa maadhimisho 
ya siku ya idadi ya watu duniani.
Waziri Ummy Mwalim (wa tatu kutoka kushoto kwa waliokaa) akiwa katika 
picha ya pamoja na wanafunzi waliohudhuri maadhimisho ya siku ya idadi 
ya watu duniani. Wa kwaza kutoka kusho ni Mkurugenzi Mkuu Ofisi ya Taifa
 ya Takwimu Dkt. Albina Chuwa, wa pili (kutoka kushoto) ni Kaim Katibu 
Mtendaji Tume ya Mipango Bibi Florence Mwanri, wa kwanza (kutoka kulia) 
ni Katibu Mtendaji Tume ya Mipango Zanzibar bw. Juma Reli na wapili 
kutoka kulia ni Mwakilishi mkazi wa UNFPA Tanzania Dkt. Natalia Kanem.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni