Na BMG 
 
Ni
 muonekano wa milima ambayo inapatikana katika Wilaya ya Rorya mkoani 
Mara, Mita chache Kutoka Mto Mara ukiwa unatoka au unaelekea wilayani 
Tarime, ukitokea maeneo mbalimbali katika barabara ya Musoma-Tarime. 
 
 Maajabu ya milima ambayo iko pande zote mbili za barabara si kwamba 
yanatisha, la hasha. Ni maajabu ambayo ni ya kufurahisha kiukweli 
hususani ukiwa safarini ambapo ukiitazama utaona namna inavyorudi nyumba
 na kufanya abiria kuhisi uumbaji wa Mungu uliotukuka katika hii dunia. 
 
 Ujenzi wa barabara iliyopinda mithiri ya nyoka katikakati ya milima hii
 huifanya kuwa kivutio kingine japo kwa abiria waoga wakifika katika 
milima hii sara huwa inaongezeka maana si mchezo hususani likija suala 
la mpando huwa ni mpando kweli, na likija suala la mtelemko huwa ni 
mtelemko kweli kwani ikiwa wewe ni muoga basi huweza hata chungulia nje 
japo ukweli ni kwamba ukichungulia nje utaona uzuri wa kipekee katika 
milima hiyo. 
 
 Kikubwa tunaomba shughuli za kibidanamu 
zisiiathiri milima hii (mfano katika picha) maana ni tegemeo kwa 
wanamara na sote twajua umuhimu wa milima kama hii ambayo ina uwepo 
mkubwa wa mistu ya a
sili. 
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni