WENYEJI UFARANSA WATINGA FAINALI EURO 2016 SASA KUIVAA URENO

Wenyeji Ufaransa wamesonga mbele na kutinga fainali za Euro 2016 kwa kupata ushindi wao wa kwanza dhidi ya Ujerumani katika michuano mikubwa ya kimataifa tangu mwaka 1958.

Mfungaji anayeongoza kufunga magoli katika michuano hiyo Antoine Griezmann, alitoa mchango muhimu katika ushindi huo katika kipindi cha kwanza na cha pili kwenye dimba la Stade de France.

Griezmann alifunga goli la kwanza kwa mkwaju wa penati katika kipindi cha kwanza, baaada ya kiungo wa Ujerumani Bastian Schweinsteiger kushika mpira na kushuhudiwa na refa Muitalia Nicola Rizzoli.

Griezmann tena aliwanyanyua mashabiki wa Ufaransa vitini na kuwahakikishia ushindi baada ya kuachia shuti la karibu, kufuatia kipa Manuel Neuer kuokoa mchomo wa Paul Pogba na mpira kumkuta mfungaji na kufanya matokeo kuwa 2-0.
                  Antoine Griezmann akipiga mkwaju wa penati uliozaa goli la kwanza
  Kipa Manuel Neuer akiwa kapotea maboya na kuruka upande mwingine mpira ukitinga wavuni
               Antoine Griezmann akifunga goli la pili dakika 18 kabla ya mpira kuisha

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni