Kipindupindu
 ni ugonjwa wa kuharisha na kutapika unaosababishwa na vimelea vya 
bacteria vinavyoitwa kwa lugha ya kitaalam “vibro cholera”. Chanzo cha 
kikubwa cha ugonjwa huu huletwa na vimelea vilivyomo kwenye kinyesi na 
matapishi ya mgonjwa wa kipindupindu.
Kwa 
miaka mingi sasa wananchi wa Tanzania tumekumbwa na magonjwa ya aina 
mbalimbali ya mlipuko ukiwemo ugonjwa wa kipindupindu ambao umeenea kwa 
kasi kubwa sana kutokana na kuwepo kwa mazingira hatarishi yanayochochea
 mlipuko wa ugonjwa huo.
Kwa 
mwaka 2015 ugonjwa wa kipindupindu umetikisa nchi yetu kwa kiasi kikubwa
 na kusababisha watu kupoteza uhai na kupunguza nguvu kazi, watoto kuwa 
yatima wake kwa waumwe kuwa wajane na wengine kuwapoteza ndugu jamaa na 
marafiki zao.
Siyo 
mara ya kwanza kutokea kwa mlipuko wa ugonjwa wa kipindupindu nchini ila
 imekuwa ni tabia ya watanzania kuchukulia mazoea na kuuona ugonjwa huu 
kama michezo ya watoto kwenye televisheni       ( TV Game) na huku miaka
 nenda rudi unazidi kuteketeza watanzania. kwanini watanzania hatulioni 
hili kuwa ni janga la kitaifa?
Ugonjwa
 wa kipindupindu ulioanza Agosti 15 2015 katika mkoa wa Dar es salaa na 
kuenea kwa kasi katika mikoa mingine 20 nchini, kwa mujibu wa taarifa ya
 tarehe 15 Desemba 2015 kumekuwa na wagonjwa wapya 141 na kufanya jumla 
ya wagonjwa waliokwa wanaendelea kupatiwa matibabu kwenye vituo vya 
kutolea huduma katika mikoa yote iliyoathirika kuwa 184 na vifo vipya 
viwili.
Tangu 
ugonjwa huu uanze jumla ya watu 11,257 walipata ugonjwa huu na kati yao 
177 wamefariki kwa ugonjwa huu ambayo ni sawa na asilimia 1.5 ya 
waliougua, mpaka sasa kwa wastani ugonjwa huu umepungua katika mikoa ya 
Dar es salaamna kwa mkoa wa Iringa na mji wa Moshi kwa kiasi kikubwa 
wamefanikiwa kudhibiti ugonjwa huu.

Katika
 tamko la Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii,Jinsia Wazee na Watoto Mhe 
Ummy Mwalimua alilolitoa tarehe 16 Desemba 2015 kuhusu mapambano ya 
ugonjwa wa kipindupindu, Waziri huyo alipiga marufuku uuzaji wa matunda 
yaliyokatwa na vyakula sehemu za wazi(barabarani) na kutoa amri 
 watakaokiuka wachukuliwe hatua mara moja.
“ 
Nahitaji nipatate taarifa ya utekelezaji kila siku kutoka kwa Waganga wa
 Mikoa na Wilaya na Serikali haitasita kuchukua hatua kwa viongozi ambao
 watashindwa kudhibiti ugonjwa huu katika maeneo yao” alisema Waziri 
Ummy katika tamko lake kupitia Vyombo vya Habari. 
Mara 
baada ya kutolewa kwa tamko hilo siku tatu baadae mwandishi wa makala 
hii nilifanya ziara ndogo kuzunguka baadhi ya maeneo ya Jiji la Dares 
salaam hasa katikati ya Jiji na kugundua kuwa bado kuna uuzaji wa 
matunda yaliyokatwa na vyakula sehemu za wazi(barabarani) unaendelea. 
Katika kufatilia hilo kujua nini Jijini limefanya hasa Manispaa ya Ilala
 ambayo ndo muhusika wa maeneo ya katikati ya Jiji niliwasiliana na 
msemaji wa Manispaa ya Ilala Bw. Daud Langa na kutoa ufafanuzi wa suala 
hilo.
Msemaji
 wa Manispaaa ya Ilala alisema katika suala hili watendaji wa kata na 
mitaa wanahusika moja kwa moja kusimamia na kufatilia kwa karibu 
operesheni hii na kusisitiza sheria za afya kuzingatiwa na hakutokuwa na
 huruma kwa yoyote atakayevunja sheria.
“ Kwa 
mfanyabiashara yoyote tutakayemkamata anauza matunda yaliyokatwa na 
vyakula maeneo ya wazi tutamkamata na kumfungulia mashtaka ya kuvunja 
sheria za Afya na adhabu yake ni faini ya Sh 30,000 au kwenda jela miezi
 mitatu au vyote kwa pamoja” alisema Langa alipokuwa akitoa maelezo 
hayo.
Nakumbuka
 Desemba 9 mwaka huu  ilitangazwa kuwa ni siku ya Uhuru na Kazi na Mhe 
Rais Dkt Jhn Pombe Joseph Magufuli na kuamuriwa iwe siku ya kufanya 
usafi katika maeneo yetu ikiwa ni mapambano dhidi ya ugonjwa wa 
kipindupindu ulioenea kwa kasi . katika ziara yangu nilipita maeneo ya 
kawe sokoni na mto Mbezi ambapo wananchi kushirikiana na watumishi wa 
taasisi za umma na binafsi walijitokeza kufanya usafi katika maeneo 
hayo.
Katika
 maeneo ya Kata ya kawe eneo la mto Mbezi watumishi wa iliyokuwa Wizara 
ya kazi na Ajira ambayo imehamishiwa Ofisi ya Waziri Mkuu na kuwa Sera, 
Kazi, Ajira, Vijana na Walemavu walijitokeza kufanya usafi 
wakishirikiana na wanachi wa maeneo hayo. Cha kushangaza ni pale 
watumishi hao walipofika na kuanza kufanya usafi na huku wananchi wa 
pale wakiwaangalia kama wafanya maonesho ya sanaa za maigizo.
Hivi 
tunasubiri waje watu toka nje ya Tanzania  watusafishie maeneo yetu 
sisemi watanzania wote ni wavivu hapana ndio wapo wachache waliobarikiwa
 kwa kuelewa nini wajibu wao katika jamii inayowazunguka lakini wachache
 pia wanaharibu sifa ya watanzania na kufanya watanzania tuonekane 
wavivu kazi kutoa lawama hata kwa yale tutanayoweza kuyafanya yaliyo 
ndani ya uwezo wetu.
Tabia 
yetu watanzania tulio wengi ni kutupia lawama na malalamiko kwa Serikali
 hivi kwani Serikali ni nani? Serikali ni mimi na wewe na yule swala sio
 Serikali imekufanyia nini ila wewe umeifanyia nini nchi yako? Suala la 
usafi liko chini ya uwezo wetu tulifanye basi kwa bidii na hatuifanyii 
serikali bali tunaifanyia nchi yetu na vizazi vyetu tukiwa na tabia ya 
usafi toka tunakoishi mitaani basi itakuwa tabia ya taifa zima kwa 
ujumla.
Watanzania
 tujilaumu wenyewe kuugua kipindupindu kwasababu tunaweza kukizuia kwa 
kuzingatia usafi wa mazingira na usafi wa mipango miji pia kutojenga 
kwenye mikindo ya maji mito na maziwa na vyanzo vya maji kwani maji ndo 
chanzo kikubwa cha kipindupindu kwani maji yanatumika kwa asilimia kubwa
 katika matumizi ya binadamu ya kila siku.
Serikali
 kwa upande wake inapambana sana na suala hili la kipindupindu kwa kasi 
kubwa kupitia wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na watoto
 ikishirikiana na Halmasahuri za Wilaya, Ofisi za Afya za Mikoa na 
Wilaya na katika kukabilana na ugonjwa huu sekta zote husika zikiwemo 
Maji, Elimu, Mawasilano, Uchukuzi na Ujenzi hazina budi kushirikiana kwa
 pamoja ili kutokomeza ugonjwa huu.
Aidha 
wadau wa maendeleo ya jamii hawakuwa nyuma kusaidia kampeni hii ya 
kutokomeza kipindupindu nchini, mashirika kama vile shirika la Afya 
Duniani (WHO), CDC, USAID, MSF, Red Cross na UNICEF kwa kushiriki katika
 kukabiliana na mlipuko huu. Kwa mujibu wa Wizara ya Afya Maendeleo ya 
Jamii, Jinsia, Wazee wadau hawa wamechangia msaada wa fedha na vifaa 
vyenye thamani ya Tsh 1,884,000,000 na serikali ikatoa Tsh 900,000,000 
katika kupambana na ugonjwa huu.
Watanzania
 tunahamasishwa kupambana na ugonjwa huu kwa kuona kuwa kipindupindu ni 
aibu kwetu mtu kuugua ugonjwa huu wakati unazuilika kwa kuzingatia usafi
 tu. Wote kwa pamoja kupitia magazeti Radio, Televisheni mitandao ya 
Jamii kama Whatsaap, Twitter na Instagram tuelimishane kuhusu usafi wa 
mazingira ili kutokomeza kpindupindu na kikwa historia nchini.
Kwa 
taarifa kuhusu ugonjwa wa kindupindu unaweza kuzipata kupitia ujumbe 
mfupi kwenye simu yako kuandika neon kipindupindu kwenda 15774 na 
utapata taarifa sahihi juu ya ugonjwa wa kipindupindu na ujembe huu 
unapatikana bila malipo. Tukumbuke kuwa kinga ni bora kuliko tiba, 
kuugua Kipindupindu ni aibu.

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni