HOSPITALI YA MOUNT MERU INAKABILIWA NA UPUNGUFU WA DAMU

Image result for damu salama picha

Na Mahmoud Ahmad Arusha
HOSPITAL ya mkoa wa Arusha, Mount Meru,inakabiliwa na upungufu mkubwa wa damu salama  kwa ajili ya kuokoa maisha ya wagonjwa wanaohitaji damu kwa ajili ya matibabu yao.

Mganga mkuu wa hospital ya mkoa wa Arusha, Dakta Frida Mokiti, amekiambia kikao cha kamati ya maafa ya mkoa wa Arusha, kuwa hospital hiyo inahitaji uniti 1560 za damu salama,lakini  akiba ya damu salama iliyopo ni uniti 40 .

Kutokana na upungufu huo, mganga mkuu wa mkoa wa Arusha Dakta Frida Mokiti, akatoa wito kwa wananchi kujitokeza kwa wingi kujitolea damu nili kuokoa maisha ya wagonjwa ambao matibabu yao yanahitaji damu salama.

Amesema upungufu mkubwa wa adamu unasababisha wagonjwa wanaosubiri matibabu yanayotegemea damu salama kuwa kwenye   wakati mugumu ili kuokoa maisha yao.

Dakta Mokiti, amewaambia wajumbe wa kikao hicho cha kamati ya maafa ya mkoa kuwa makundi makubwa yenye uhitaji mkubwa wa damu salama kwenye matibabu yao ni  wajawazito, watoto na majeruhi .

Wajumbe wa kikao hicho ni pamoja na katibu tawala mkoa, wakuu wa wilaya, wakurugenzi, wenye viti, madaktari wa wilaya na mkoa,sekretarieti ya mkoa,na wataalamu wa ngazi mbalimbali na maafisa afya .

 Dakta Mokiti,  amesema akiba ya damu salama iliyopo ni kidogo sana kuokoa maisha ya wagonjwa ambao matibabu yao yanahitaji damu nyingi,hivyo anaomba wananchi kujitokeza kuchangia damu ili kuokoa maisha ya wagonjwa.

Dakta, Mokiti, amesema mahitaji makubwa ya damu salama yanatokana na wingi wa wagonjwa wanaofika hospitalini hapo  hospital  kwa ajili ya matibabu yao,na pia hospital hiyo ya mkoa ndio inategemewa na hospital zingine kupata damu.

 Kwa upande wake kaimu katibu tawala wa mkoa huo,  Anza Amen Ndosa,aliwataka wakurugenzi wa haslmashauri za wilaya walifanyie kazi na wasitumie bajeti kama visingizio ili kukwepa jukumu la kuchangia damu salama kupita kwenye halmashauri zao.

Amesema uhai wa binadamu hautegeme bajeti bali damu hivyo  akazitaka halmashauri kuhamasisha wananchi kujitolea damu ili kuwezesha kupatikana akiba ya damu salama  ili kuokoa maisha ya wagonjwa ambao matibabu yao yanategemea damu.

Nae mwenyekiti wa  Chama cha msalaba mwekundu mkoa wa Arusha,Dakta Christopher Nzela, amekiambia kikao hicho kuwa Msalaba mwekundu,kimekuwa kikishiriki kuhamasisha wananchi kujitolea kuchangia damu salama kwa ajili ya kuokoa maisha ya wagonjwa wanafikishwa vhospitalini kwa matibabu .

Hamasa hiyo inayotolewa na msalaba mwekundu, imekuwa ikisaidia kupatikana damu salama kutoka kwa wananchi wachache wanaojitokeza kujitolea damu kwa ajili ya kuokoa maisha ya wagonjwa.

Nzera, amesema mwamko mdogo wa wananchi imekuwa ni changamnoto kubwa ya kufikia malengo ya upatikanaji wa damu salama na hilo linatokana na kuwa na uelewa mdogo na kutokujiamini kiafya.

Inawezekana wananchi walio wengi hawana uelewa wa kujitolea kuchngia damu salama,wengine hawajiamini hivyo wanakuwa na hofu ya damu zao kukutwa na maambukizi  ya virusi vya ugonjwa wa Ukimwi hivyo inakuwa vigumu kujitolea kutoa damu.

Nzera, amesema msalaba mwekundu mkoani Arusha,imekuwa ikihamasisha  vijana wa shule za sekondari na vyuo ambao huwa wanakuwa na mwamko mkubwa wa kujitolea damu salama,wakati makundi mengine ya kijamii yakiwa hayashiriki. MWISHO
 
Arusha.
SERIKALI Nimewahakikishia wananchi kuwa ulinzi na usalama umeimarishwa kwenye kipindi chote cha siku kuu na hivyo kutoa fursa kwa wananchi kusherehekea sikuu kuu zote bila hofu.

Mkuu wa mkoa wa Arusha, Felix Ntibenda, ameyasema hayo jana alipokuwa vakizungumza na vyombo vya habari ofisini kwake na kuelezea hatua zinazochukuliwa na serikali kuimarisha usalama wa wananchi na kuhakikisha kuwa usalama wa kutosha upo.

Amevipongeza vyombo vya dola ambavyo vimekuwa vikiimarisha ulinzi na kuwezesha wananchi wanaishi kwa usalama na amani kwa kuzuia matukio yeyote ya uhalifu yaliyokuwa yakitishia usalama na uhai wa wananchi na mali zao.

Kuhusu utunzaji wa mazingira, Ntibenda, amesema kuwa tayari ameshaziagiza wilaya zote kupanga mpango kazi wa kupanda miti mwaka 2016, ili kuondoa tatizo la uharibifu wa mazingira na ukame unaosababisha na ukosefu wa mvua.

Amesema katika kuhakikisha agizo hilo linatekelezwa kila mkuu wa wilaya atalazimika kufuatilia kila kaya kuhakikisha imepanda miche 30 aina mbalimbali na kuitunza ili ikue .
      MWISHO.
      ARUSHA.
CHAMA cha msalaba mwekundu, mkoa wa Arusha, kimekuwa kikishiriki kikamilifu kwenye mapambano ya kutokomeza ugonjwa wa kipindu pindu ambao umedumu kwa kipindi kirefu mkoani Arusha.

Mwenyekiti wa Msalaba mwekundu mkoa wa Arusha, Dakta Chirstopher Nzera, amesema kuwa Chama hicho kiliitikia wito wa serikali ya mkoa ya kuomba wadau kusaidia mapambano ya kutokomeza ugonjwa huo.

Amesema Chama  kimekuwa kikiwatumia wanachama wake kwa kujitolea  ambao wamekuwa wakishiriki mapambano hayo kwa kushiriki kusafisha maeneo mbalimbali jijini Arusha na halmashauri ya Arusha DC.

Amesema Msalaba mwekundu,kinashiriki kwenye zoezi la kupulizia dawa za kuuwa wadudu mbalimbali kwenye nyumba,kupulizia dawa kwenye visima vya maji,pia kupulizia dawa kwenye vyombo vya usafiri vya abiria,na kutembelea vituo vya biashara ambako chama kimekuwa kikitoa elimu ya kujikinga na kuchukua hatua za maambukizi ya ugonjwa huo .

Nzera, alikuwa akitoa taarifa fupi ya utendaji kwenye kikao cha kamati ya maafa ya mkoia wa Arusha kilichofanyika jana  na kuongeza kuwa Msalaba mwekundu inakusudia kushiriki kwenye zoezi hilo kwa wilaya zote za mkoa bwa Arusha.
      Mwisho.
      ARUSHA.
 
MAMLA ya maji safi na taka jijini Arusha,imeahidi  kuboresha huduma ya maji safi kwenye maeneo yote ambayo hayana maji ilkiwa ni hatua za kukabiliana na maambukizi ya ugonjwa wa kipindu pindu.

Mkurugenzi mtendaji wa AUWSA, mhandisi Ruth Koye, ametoa ahadi hiyo jana kwenye kikao cha kamati ya maafa ya mkoa na kuahidi kuwa  maeneo ambayo hayapati maji ya mtandao wa AUWSA, na kusababisha wananchi kutumia majhi yasiyo salama watapata maji ya AUWSA.

Amesema AUWSA, inaboresha huduma ya maji kwa awamu lengo ni kuhakikisaha wananchi wanapata huduma hiyo ya maji safi na hivyo kuwawesha kuepukana na ,maambukizi ya kipindu pindu kinachotokana na matumizi ya maji yasiyo safi na salama .

Kikao hicho kiliagiza AUWSA,kuhakikisha maji yanapatikana maeneo yote ambayo hayana maji ili kupunguza tatizo la kuenea kwa ugonjwa wa kipindu pindu.

Aidha kikao hicho pia kimelitaka shirika la umeme nchini Tanesco,mkoa wa Arusha, kuhakjikisha umeme kwenye vyanzo vya maji vya AUWSA, haukatiki ili kuwezesha AUWSA, kuzalisha maji ya kutosha wakati wote .

Kikao kimesema kukatika mara kwa mara kwa umeme kwenye vituo vya kuzalisha maji vinasababisha AUWSA, kutokusambaza maji ya kutosha na hivyo kuwepo mgao wa maji kwa maeneo mengi ya jiji la Arusha.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni