SERIKALI MKOANI HAPA YAFUTA LIKIZO ZA WATUMISHI WAKE


Image result for picha rc arusha

 Na manyara leo blog Arusha
SERIKALI ya mkoa wa Arusha imefuta likizo zote za watumishi ambao walikuwa wakitarajia kwenda mapumzikoni na kuwataka waendelee na kazi kwa kushiriki  kwenye mapambano ya kutokomeza ugonjwa wa kipindu pindu ambacho kimeendelea kuwepo mkoani Arusha.

Mkuu wa mkoa wa Arusha, Felix Ntibenda, maarufu kijiko, ametoa maelezo hayo alipokuwa akiahirisha kikao cha kamati ya maafa ya mko, na kusisitiza hakuna likizo mpaka kipindu pindu kitakapotokomezwa .

Amesisitiza Kwenye hotuba yake iliyosomwa na mkuu wa wilaya ya Arusha, Fadhili Nkurlu, mkuu wa mkoa amesema hadi Desemba 23 kuna wagonjwa 14 ambao wamelazwa kwenye vituo mbalimbali na kusisitiza kuwa Arusha bila kipindu pindu inawezekana hivyo watunishi na wananchi kwa pamoja lazima kushirikiana ili kuondoa kabisa ugonjwa huo.

Ntibenda,amesema swala la kudhibiti ugonjwa huo linaonekana kuachiwa idara ya afya pekee ambayo haiwezi kukabiliana na mlipuko wa ugonjwa huo hivyo sewkta zote lazima kushirikiana kuutokomeza .

Akawawaomba viongozi wa kisiasa, kijamii, kimila  kushiriki kikamilifu  kwenye mapambano hayo  kwa kuwa ugonjwa wa kipindu pindu hauna itikadi , hivyo akatoa wito kutolewa taarifa haraka pindi kunapotokea mgonjwa au mwenye dalili za ugonjwa wa kipindu pindu .

Pia Ntibenda, akahimiza matumizi ya vyoo pamoja na kuimarisha usafi wa mazingira ,sanjari na kuwachukulia hatua wale wote watakaokuwa ni chanzo cha uchafuzi wa mazingira na kusababisha kuendelea kuwepo kwa ugonbjwa huo.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni